Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Zaidi ya sh milioni 10zatengwa kufuturisha mkoa wa Dar es salaam

Zaidi ya sh milioni 10zatengwa kufuturisha mkoa wa Dar es salaam


Zaidi ya sh milioni 10 zimetengwa kwa ajili ya kufuturisha watu
wenye kipato cha chini kwenye
mwezi huu wa mfungo wa Ramadhani katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Dar
es Salaam.
 Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dar es Salaa leo,
Mwenyekiti wa Taasisi ya Al Madina, Sheikh Ally Mubaraka alisema hayo wakati alipokuwa
akipata futari kwa pamoja na  waislamu wa Msikiti wa Sheikh Gorogosi, Tandika kwa Maguruwe.
 Alisema fedha hizo zimepatika kutokana na ushirikiano mzuri
uliyopo kati ya Ubalozi wa Emirate na taasisi hiyo inayojihusisha na utoaji
misaada katika jamii yenye mahitaji maalum.

Sheikh Mubaraka alisema taasisi hiyo inalenga kutoa futari
kwenye makundi ya watu ikiwa ni ishara ya huruma kama dini hiyo inavyoelekeza.
 “Ubalozi wa Emirate umejitolea fedha za kutosha kwa ajili kufuturisha
ambapo leo (jana), tumeanzia Tandika, mpango huu ni wa kila mwaka na utafika
katika maeneo yote ya mkoa wa Dar es Salaam”alisema Sheikh Mubaraka.
 Sheikh Mubaraka aliwaasa wafanyabiashara kuacha kupandisha bei
za bidhaa kwa ajili ya kujipatia kipato kikubwa ambapo sheria za dini zinawataka
wanadamu kuoneana huruma wakati wote.
 Vilevile
alisema mwezi huu wa mfungo Ramadhani ni fursa njema ya kufanya ibada kitendo
ambacho kitawasidia waislam kufutiwa dhambi zao.
 “Yule mwenye
kula mchana katika mfungo huu,hata kama atakuwa akijibidiisha na swala atambuwe
kuwa hatoweza kufutiwa dhambi zake”alisema Sheikh Mubaraka.
 Akizungumzia
tukio la kuzama kwa meli ya Skagit, alisema taasisi hiyo imetoa pole kwa
familia zote zilizopoteza ndugu zao kwani tukio lile ni kubwa ambapo uchungu
wake umemgusa kila mtu katika nchi hii.



0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa