WAKATI
bado kukiwa na sinto fahamu juu ya hatma ya Chuo cha Sayansi ya Tiba
cha IMTU ambacho kinakabiliwa na tuhuma ya kuhusika na utupaji wa viungo
vya Binadamu vilivyokuwa vikitumika katika mafunzo chuoni hapo hivi
karibuni Hospitali yake ya IMTU imefungiwa.
Hospitali
ya IMTU iliyopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam imefungiwa kufanya
kazi zake kutokana na makosa mbali mbali ya kiutalaam lakini kubwa ni
kukosa wafanyakazi wa kutosha na kutoa huduma bila ya kuwa na vifaa
stahiki huku wakitumia madawa ambayo yamepitwa na muda wake.
Hatua
hiyo imekuja siku chache baada ya kufanyika kwa ukaguzi Hospitalini
hapo na vyanzo vinapasha hilo halina uhusiano na upande wa Chuo cha IMTU
ambao unatuhumiwa kutupa viungo vya binadamu vuilivyokuwa vikitumiwa
katika mafunzo chuoni hapo.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment