Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » AKIDI YAKWAMISHA BUNGE LA EALA

AKIDI YAKWAMISHA BUNGE LA EALA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Kutotimia kwa akidi ya wabunge wa Rwanda kulisimamisha kwa dakika 15 kikao cha Bunge la Afrika Mashariki (Eala) kilichoanza jana jijini hapa.
Ikiwa ni kikao chake cha kwanza baada ya kufunguliwa rasmi juzi, Bunge hilo lilikuwa na ajenda mbili, zote zikiwa ni uwasilishaji wa ripoti za kamati za kilimo, utalii na maliasili pamoja na ya usuluhishi wa migogoro.
“Naomba mwongozo wako Spika. Inakuwaje tunaendelea na kikao ambacho kitapitisha hoja hii wakati akidi ya wabunge kutoka Rwanda haijatimia?” alihoji Nusra Omar kutoka Uganda.
Spika Margaret Zziwa alilazimika kuita majina ya wajumbe wote wa Bunge hilo ili kujiridhisha. Alisema kutokana na kanuni za Bunge hilo, alilazimika kulisitisha ili kutoa muda kwa wasiokuwepo kama hawako mbali waingie ukumbini.
Kutokana na hilo, Zziwa alitoa mwongozo kuwa “Kanuni Namba 13 ya Mwenendo wa Eala inasema ili kikao cha Bunge kiendelee, lazima kuwe na nusu ya wabunge waliochaguliwa ambao watajumuisha wajumbe watatu kutoka katika kila nchi wanachama. Hivyo naliahirisha Bunge hili kwa dakika 15”.
Bunge hilo linafanyika jijini hapa kwa mara ya kwanza tangu utaratibu wa kufanya vikao vyake katika miji tofauti ya nchi wanachama upitishwe. Hata hivyo, baadhi ya wajumbe wamedai kuwa hiyo ni njama ya Rwanda kutotaka vikao hivyo vifanikiwe.
 Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa