Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » KUWA NA WATOTO WENGI HUCHANGIA UMASIKINI-UTAFITI

KUWA NA WATOTO WENGI HUCHANGIA UMASIKINI-UTAFITI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Ukubwa wa familia unachangia zaidi umaskini nchini, Benki ya Dunia (WB) imeeleza.
Kwa mujibu wa ripoti ya benki hiyo, mambo mengine yanayochangia umasikini kwa mujibu wa ripoti hiyo ni kiwango cha elimu, miundombinu, ajira na kuhama makazi.
“Familia zenye watoto zaidi ya kumi kwa mwaka 2012, ni masikini kwa asilimia 45. Kiwango hicho kimeongezeka kutoka asilimia 42 kwa mwaka 2007. Kiwango cha umasikini kwa familia zenye watoto chini ya watatu ni chini ya asilimia 20,” inaeleza ripoti hiyo.
Akizungumzia ripoti hiyo, Dk Adolf Mkenda, kaimu katibu mkuu wa Wizara ya Fedha, alisema: “Ni kweli familia zenye watoto wengi zinashindwa kutimiza mahitaji yote ya msingi. Wazazi wanaelemewa katika matibabu, ada, chakula na wakati mwingine malazi.”
Mkurugenzi mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk Albina Chuwa alisema: “Njia pekee ya kuondokana na umaskini katika familia yenye watoto wengi ni kuongeza uwekezaji ili kukidhi mahitaji ya kila mwanafamilia kama walivyofanya India.”
Ukiacha ukubwa wa familia, kiwango cha elimu kinashika nafasi ya pili kwa kuchangia umaskini.
Ajira zenye mshahara zimeelezwa kupunguza umaskini.
Ripoti hiyo inaeleza kuwa watumishi wa Serikali ndio wanaoongoza katika kupunguza kiwango cha umaskini kutokana na kunufaika na mishahara.
Inaeleza kuwa kiwango cha umaskini kwa watumishi wa Serikali ni asilimia 7 wakati waliojiajiri wamepunguza kiwango cha umaskini kwa asilimia 32.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa