Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » ‘MIGOGORO YA KISIASA KIKWAZO KATIKA UWEKEZAJI’

‘MIGOGORO YA KISIASA KIKWAZO KATIKA UWEKEZAJI’

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Migogoro ya kisiasa katika nchi nyingi za Afrika ni miongoni mwa sababu inayokwamisha uwekezaji kutoka nje na jitihada za kupambana na umaskini na ukuzaji wa uchumi wa mataifa hayo.
Akizungumza wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika jijini hapa jana, makamu wa rais wa Taasisi ya Kudhamini Uwekezaji (Miga), Michael Wormser alisema machafuko ya kisiasa yanafanya wawekezaji wengi kuogopa kufanya hivyo barani Afrika.
“Hatari ambazo zinawapa wasiwasi wawekezaji na wakopeshaji mara nyingi zinahusiana na imani ndogo katika mifumo ya mahakama na taasisi za udhibiti, utawala mbovu, rushwa na uhaba wa utawala wa sheria,” alisema.
“Kinachotokea hivi sasa katika nchi nyingi ni kutokuwapo kwa usimamizi wa mikataba, machafuko ya kisiasa na kuyumba kwa uchumi mkuu wa nchi husika.”
Alisema nchi nyingi za barani Afrika zinakabiliwa na uwekezano mkubwa wa kupoteza mitaji ambayo ni muhimu katika ukuzaji wa uchumi. Alisema Tanzania ina usalama na fursa nyingi za uwekezaji zikitumiwa vizuri
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa