Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » KUBENEA KWENDA MAHAKAMA YA RUFANI

KUBENEA KWENDA MAHAKAMA YA RUFANI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Saed Kubenea
 
Wakili Peter Kibatala wa mlalamikaji kuhusu madaraka ya Bunge Maalum la Katiba, Saed Kubenea, amedai kuwa anataka kuwasilisha nia ya kukata Rufaa Mahakama ya Rufani Tanzania, kupinga uamuzi uliotolewa na Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kibatala, anakata rufaa kupinga sehemu ya uamuzi wa Mahakama Kuu katika kipengele kinachoeleza  kwamba pamoja na kwamba Bunge Maalum la Katiba lina mipaka na linatakiwa kutekeleza mamlaka yake kupitia  Rasimu na kifungu cha 9 (2).

Sababu nyingine ya kukata rufaa ni  kwamba baada ya kusema Bunge Maalum la Katiba  linaweza kurekebisha  na kuboresha Rasimu, Mahakama ilitakiwa kusema kwamba marekebisho na maboresho ni tofauti na kutoa kabisa vifungu kadhaa kuwa suala la uwazi.

“Tutawasilisha nia ya kukata rufaa Mahakama ya Rufani wakati tukisubiri  Oktoba 7, mwaka huu kusomewa hukumu ya jumla ya maombi ya kuhoji uhalali na mamlaka ya Bunge hilo,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

 Pamoja na mambo mengine, Kibatala kupitia taarifa yake alisema ataangalia pia uwezekano wa kufungua shauri chini ya hati ya dharura katika eneo fulani la mchakato na kwamba ni muhimu kuishirikisha Mahakama.

Aidha, aliishukuru Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam  kwa kile ilichofanya kwa uwezo wake, na imechangia sana maendeleo ya sheria na ya mchakato mzima, lakini bado kuna kiu katika maeneo waliyoiainisha na wanaona rufaa ni muhimu.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa