Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » NEC YAANZA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGAKURA

NEC YAANZA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGAKURA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
KURA YA MAONI: Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (Nec), Hamid Mahamudu Hamid akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana. Kulia ni Mkurugenzi Uboreshaji wa Daftari la Wapigiakura, Julius Malapa
 Kitendawili cha tarehe rasmi ya Watanzania kupiga Kura ya Maoni itakayopitisha au kukwamisha KatibaInayopendekezwa, kitateguliwa kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(Nec) baada ya kukamilisha uboreshaji Daftari la Kudumu la Wapigakura Aprili mwaka ujao.
Nec imebainisha hayo jijini Dar es Salaam jana ikieleza kuwa  tayari Serikali imetoa Sh15 bilioni za uboreshaji huo na kwamba utakamilika Serikali itakamilisha kutoa Sh270 bilioni zinazohitajika kwa ajili ya uboreshaji wa daftari hilo.
Hadi sasa, kuna mkanganyiko kuhusu tarehe hiyo baada ya Rais Jakaya Kikwete kutaja mwezi Aprili  mwakani kama wakati wa kupiga kura hiyo, akipingana na Machi 15 iliyotolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema. 
Makamu mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Hamid Mahmoud Hamid, alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa tume hiyo itakamilisha daftari hilo ifikapo Aprili mwakani.

‘’Mpaka sasa Serikali   imeshatoa Sh15 bilioni, tutaendelea kupokea kidogo kidogo kutoka Hazina. Ikiwa zikifika kwa wakati, tutakamilisha zoezi hili Aprili 18 mwakani,’’ alisema na kuongeza: ‘’Mtakumbuka awali tuliarifu wananchi kuwa zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura lingeanza Septemba mwaka huu, hata hivyo halikuanza kutokana na kuchelewa kupatikana kwa fedha kutoka serikalini.’’
Alisema kuwa kwa sasa Nec imeanza kupewa fedha na Serikali  kuwawezesha kuanza kwa zoezi hilo la uboreshaji daftari hilo.
Jaji Hamid aliongeza kwamba mara baada kupokea kiasi hicho pamoja na vifaa vya uboreshaji wa daftari hilo, Nec ilianza kutoa mafunzo kwa watendaji wake.
“Novemba mwaka huu, tutafanya majaribio ya uboreshaji daftari la wapigakura kutumia mfumo wa ‘Biometric Voter Registration’ katika majimbo matatu ya uchaguzi ya Kawe Manispaa ya Kinondoni, Halmashauri ya Mji wa Kilombero na Mlele Halmashauri ya Mji wa Katavi,” alisema.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa