Mwenyekiti wa mtandao wa Redio Jamii nchini (COMNETA) ambaye pia ni
Mkurugenzi wa Redio ya Jamii ya Wilayani Karagwe ya FADECO FM, Bw.Joseph
Sekiku akizungumza katika hafla fupi ya kumuaga Makamu Mkuu wa Chuo
Kikuu Huria Tanzania (OUT) ambaye amemaliza muda wake, Prof. Tolly
Mbwete (katikati) iliyoandaliwa na Mtandao wa Redio za Jamii nchini
(COMNETA). Kushoto ni Mshauri na Mkufunzi kutoka Shirika la Umoja wa
Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose Haji Mwalimu.
Katibu
wa mtandao wa Redio Jamii nchini (COMNETA), Riziki Leisuya akisoma
risala fupi wakati wa hafla ya kumuaga Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria
Tanzania (OUT), Prof. Tolly Mbwete.
Mkuu
wa Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT) ambaye amemaliza muda wake, Prof.
Tolly Mbwete akipokea risala iliyosomwa na Katibu wa mtandao wa Redio
Jamii nchini (COMNETA), Riziki Leisuya wakati wa hafla fupi ya kumuaga
iliyoandaliwa na WanaCOMNETA.
Makamu
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania ambaye amemaliza muda wake, Prof.
Tolly Mbwete (wa pili kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Mhariri wa
Sibuka FM, Anita Balingilaki kwa niaba ya Wanamtandao wa Redio Jamii
nchini Tanzania (COMNETA) kama ishara ya kumuaga rasmi wakati wa hafla
fupi iliyoandaliwa na wanamtandao huo ya kumtaki kheri katika majukumu
mapya anayoenda kufanya nchini Addis Ababa.
Kushoto
ni Mshauri na Mkufunzi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu,
Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose Haji Mwalimu na Wa pili kulia ni
Mwenyekiti wa mtandao wa Redio Jamii nchini (COMNETA) ambaye pia ni
Mkurugenzi wa Redio ya Jamii ya Wilayani Karagwe ya FADECO FM, Bw.Joseph
Sekiku akifutiwa na Mshauri wa UNESCO, Balozi mstaafu Mh. Christopher
Liundi.
Mshauri wa UNESCO, Balozi mstaafu Mh. Christopher Liundi akitoa wasifu wa Prof. Tolly Mbwete kwenye hafla hiyo fupi.
Makamu
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT) ambaye amemaliza muda wake,
Prof. Tolly Mbwete katika picha ya pamoja na wakufunzi na washiriki wa
warsha ya siku tatu kutathmini mradi wa demokrasia na Amani (DEP) yenye
lengo la kuimarisha ushiriki wa redio za jamii nchini kuelekea uchaguzi
2015 na kura ya maoni kwa wanamtandao wa Redio Jamii nchini (COMNETA)
iliyoendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu,
Sayansi na Utamaduni (UNESCO) na kufadhiliwa na Shirika la Umoja wa
Mataifa la Maendeleo (UNDP) ambayo imemalizika mwishoni mwa juma katika
ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria (OUT).
MTANDAO
wa Radio za Kijamii nchini Tanzania (COMNETA) na Chuo Kikuu Huria (OUT)
kwa umoja wao zimepongeza mchango mkubwa wa aliyekuwa Makamu Mkuu wa
chuo hicho Profesa Tolly Mbwete kwa jitihada zake za kuziunganisha redio
jamii na chuo kuhakikisha taarifa zinawafikia walio wengi hasa
vijijini.
Katika
hafla fupi iliyofanyika katika ukumbi wa OUT hivi karibuni mtandao wa
COMNETA umesema jitihada za Profesa Mbwete kuziunganisha taasisi hizo
mbili zimefanikishwa kwa kiasi kikubwa kufikisha taarifa za kozi
mbalimbali zinazoendesha chuoni na kwa bei nafuu kwa Watanzania wengi
ambao umesaidia kukifahamu na hatimae kujiunga na chuo.
Akisoma
risala fupi iliyotayarishwa na COMNETA, Katibu wa mtandao huo Riziki
Leisuya alisema kwamba makubaliano na mashirikiano kati ya Comneta na
OUT yaliyowezeshwa na Profesa Mbwete yamezaa matunda mengi baina ya
pande hizo mbili kiasi cha kulishawishi Shirika la Umoja wa Mataifa la
Elimu ,Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kukubali kujenga studio ya redio
katika chuo hicho ili kurahisisha mawasiliano kwa kutayarisha vipindi
lakini pia itatumika na wanafunzi wanaochukua taaluma ya uandishi
kufanya mazoezi kwa vitendo kuboresha mafunzo yao.
“Comneta
kupitia redio zake imefanikiwa kupeleka habari wilayani na vijijini kwa
kukitangaza chuo kwa watu wasiojiweza jambo ambalo limesababisha
ongezeko la idadi ya wanafunzi chuoni hapo kutokana na unafuu wa
gharama” iliongeza risala hiyo iliyosomwa na Riziki.
Profesa
Mbwete ambaye muda wake wa utumishi chuoni hapo umefikia kikomo kwa
sasa amechaguliwa kuwa Mkuu wa Vyuo Vikuu vya Kikanda (Pan African
Universities-PAU) na Umoja wa Nchi huru za Afrika kuanzia mwezi Januari
mwaka 2015.
Akiwashukuru
na kuwaaga wana-Comneta ambao walihudhuria ulingo wa siku tatu
kutathminimradi wa demokrasia na Amani (DEP) Profesa Mbwete alisema
amefarijika na ushirikiano uliopo kati ya taasisi hizo mbili ambao
umekuwa na mafanikio ya kipekee kwa umma wa Tanzania na kuahidi
kumkabidhi atakayechukua nafasi yake kuendeleza ushirikiano huo na
kumshauri ofisi ya COMNETA iendelee kwa mkataba wa ushirikiano kwa miaka
mitatu na kila mwaka kuufanyika mapitio na mrejesho.
Naye
Balozi Christopher Liundi ambaye ni mshauri wa Unesco akimzungumzia
Profesa Mbwete alisema kwamba Profesa Mbwete anastahili pongezi kutokana
na jinsi alivyoimarisha Chuo Kikuu Huria na kuimarisha ushirikiano kati
ya Chuo hicho na Comneta kwa kutoa ofisi ambayo mtandao wa redio za
jamii unaitumia kwa kutekeleza majukumu yake kama jitihada za kutoa
uwezo kwa mtandao huo.
“Profesa
Mbwete alikuwa mstari wa mbele kupanua chuo na namshukuru sana kwa
kauli yake ya kuipa COMNETA miaka mingine mitatu kutumia ofisi
iliyotolewa na chuo chini ya usimamizi wake. Ninaamini kwamba huko
aendako atapeperusha bendera ya Tanzania na ataiwakilisha vizuri kwenye
PAU, nina matarajio makubwa sana kutoka kwake,’ alisema Balozi
Christopher Liundi.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment