Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Rais Dr Kikwete akipata maelezo ya bidhaa za Asas Daireis Ltd kampuni hii ni ndio kampuni bora ya usindikaji maziwa nchini Tanzania kwa miaka mitatu mfululizo sasa |
Rais Dr Kikwete akitazama baadhi ya bidhaa zenye ubora za kampuni ya Asas Daireis Ltd |
Rais Dr Kikwete akifurahia baada ya kutembelea banda ya Asas DaireisLtd jijini Dar es Salaam |
Wananchi mbali mbali wakitembelea banda ya Maziwa ya Asas katika viwanja wa Sabasaba jijini Dar es Salaam |
Na MatukiodaimaBlog
BANDA la kampuni ya maziwa ya Asas Dairies Ltd ya mkoani
Iringa lililopo limeendelea kuwavuta wananchi na viongozi mbali mbali wanaotembelea viwanja wa Saba saba jijini Dar e Salaam kulitembelea kupata bidhaa zake
Banda hilo ambalo wiki iliyopita lilitembelewa na Rais Dr Jakaya Kikwete na viongozio mbali mbali limeendelea kuvutia wananchi wengi wanaotembelea maonyesho hayo kupenda kufika kupata bidhaa mbali mbali .
Baadhi ya wananchi waliofika katika banda hilo walisema kuwa wamevutiwa zaidi ya bidhaa zenye ubora zinazotengenezwa na kampuni hiyo ya Asas Dairies Ltd kutoka mkoani Iringa na hivyo kulazimika kumiminika zaidi kupata bidhaa pamoja na kupata elimu mbali mbali ya ubora wa bidhaa hizo .
Alisema Amina Athuman ambae ni mmoja wa wateja waliofika katika banda hilo kupata bidhaa mbali mbali , kuwa yapo makampuni mengi ya maziwa ila ubora wa bidhaa za maziwa zinazotengenezwa na kampuni hiyo ya Asas Dairies Ltd ndizo ambazo zinawavutia watu wengi zaidi kufika katika banda hilo.
" Mimi nilikuwa nasikia tu juu ya ubora wa maziwa haya toka mkoani Iringa ila baada ya kufika hapa nimeshuhudia na kuanzia leo sihitaji maziwa na bidhaa nyingine kama hizi nje ya Asas Dairies Ltd "
Huku John Mwene akieleza kufurahishwa zaidi na hatua ya Rais wa nchi Dr Kikwete kutembelea mabanda ya wakulima mbali mbali likiwemo banda hilo la Asas kwani ni ukweli usiopingika kuwa kwa Tanzania kampuni hiyo ya Asas Dairies Ltd imeonyesha uwezo mkubwa wa kuzifanya bidhaa zake kuendelea kuwa na ubora kwa miaka mitatu mfululizo.
Kwani alisema kampuni kuongoza miaka mitatu mfululizo ni jambo la kujipongeza na kuwa si rahisi kwa kampuni kushikilia ubora wake kwa miaka miwili mfulilizo ila kampuni hiyo imeweza kufanya hivyo .
Alisema ni jambo la nchi kupitia bodi ya maziwa na wizara husika kuangalia kutoa uwezeshaji zaidi kwa makampuni bora ili kuwezesha bidhaa zake kuingizwa katika soko la dunia .
Afisa masoko wa kampuni hiyo ya Asas Dairies Ltd Bw Jimmy
Kiwelu pamoja na kumpongeza Rais Dr Kikwete kwa kutembelea banda lao na kupongeza kwa ushiriki na ubora wa bidhaa zao bado aliwashukuru wananchi wanaoendelea kutembelea banda hilo .
Alisema kuwa mbali ya kampuni hiyo kuonyesha ushiriki mzuri katika maonyesho hayo ya saba saba bado wamekuwa wakishiriki maonyesho mbali mbali yakiwemo yale ya nane nane kwa kushiriki katika kanda mbali mbali na kuwataka wananchi wa kanda zote nchini kujipanga kwa ajili ya kutembelea mabanda yao wakati wa nane nane mwaka huu .
Kuhusu kuendelea kuongoza kwa ubora alisema kuwa hivi sasa ni mwaka wa tatu mfululizo bado bidhaa zao nyingine zimeendelea kushinda
medali mbali mbali na kuonyesha uwezo mkubwa wa kampuni hiyo katika
ubora .
0 comments:
Post a Comment