Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
WAZIRI Mkuu wa zamani Mh. Edward
Lowassa, (kulia), akionyesha mkoba wenye fomu za kuomba kuwania urais
kupitia CHADEMA, baada ya kukabidhiwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Mh.
Freeman Mbowe, kwenye makao makuu ya chama hicho, Kinondoni jijini Dar
es Salaam, leo Julai 30, 2015. Mh Lowassa, alijiunga hivi karibuni na
chama hicho, baada ya kujitoa CCM.
Waziri
Mkuu Mstaafu Edward Lowassa leo amechukua fomu ya kugombea urais kwa
tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema. Lowassa amechukua
fomu hio Makao Makuu ya Chadema Kinondoni jijini Dar es Salaam na
kulakiwa na mamia ya wanachama wa Chadema na viongozi wa juu wa Chama
hicho.
Lowassa akiwasili makao makuu ya Chadema hii leo ikiwa ni siku chache baada ya kujiunga na chama hicho.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akizungumza jambo na Edward Lowassa.
Lowassa akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Chadema.
Naibu Katibu Mkuu, Salum Mwalimu akiteta jambo na Edward Lowassa.
Lowassa akisalimiana na wanachama wa Chadema.
Wana Chadema wakimlaki Lowassa.
Lowassa na ujumbe wake wakiwa katika ofisi ya Mwenyekiti kuchukua fomu.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akizungumza jambo baada ya kumkabidhi fomu Edward Lowassa kugombea Urais.
Edward Lowassa akizungumza jambo.
Lowassa na Tundu Lissu wakifurahia jambo
Lowassa akiondoka baada ya kuchukua fomu.
Kwa hisani ya Father Kidevu Blog
0 comments:
Post a Comment