Mafundi kutoka
kampuni ya Philips wanaendelea na matengenezo ya mashine za MRI na CT-SCAN
katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili zilizopata hitilafu za kiufundi hivi
karibuni.
Akizungumza ofisini
kwake leo hii Mkuu wa Idara ya Uhusiano Hospitali ya Taifa Muhimbili Bw.
Aminiel Buberwa Aligaesha amesema mafundi wapo katika eneo la kazi
wakitengeneza hizo mashine ili ziweze kurudi katika hali yake ya kawaida.
“Tumepewa siku tatu
kukamilisha ukarabati wa hizi mashine hivyo wananchi wawe na subira kwani
mashine zikiwa tayari kwa matumizi tutatoa taarifa” alisema Aligaesha.
Ameongeza kuwa wananchi
wawape muda waweze kuzitengeneza mashine hizo ili ziweze kutengemaa kwa ajili
ya kutoa huduma za MRI na CT-SCAN hospitalini hapo.
Mashine za MRI na
CT-SCAN zilianza kufanya kazi mara baada
ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Joseph Magufuli
kutembelea hospitali hiyo hivi karibuni na kuagiza kutengenezwa kwa mashine
hizo na baadae kufanya kazi kwa muda wa siku kadhaa na kuharibika tena kutoka
na hitilafu za kiufundi.
Wakati alipotembelea
Hospital ya Taifa ya Muhimbili jana Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue aliagiza
mashine hizo kutengenezwa, ndani ya siku
tatu ziwe zimekamilika kwa ajili ya
kutoa huduma kwa wananchi.
Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili imekuwa ni kimbilio la wananchi wengi kupata huduma za afya hivyo
serikali inapamabana kwa kila hali kuhakikisha huduma za MRI na CT-SCAN
zinarudi katika hali yake ya kawaida hospitalini hapo.
0 comments:
Post a Comment