Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Sababu za uharibifu wa vivuko zatajwa‏

Sababu za uharibifu wa vivuko zatajwa‏

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +25765056399. 
Na Jovina Bujulu

Uchafuzi wa mazingira katika vituo vya vivuko , utegaji wa nyavu katika njia za vivuko na kukauka kwa maji na kujaa mchanga kwenye njia za vivuko ni sababu zinazochangia kuharibika kwa vivuko nchini.

Hayo yamesemwa leo  jijini Dar es salaam na Mkurugenzi wa Ukodishaji mitambo na Huduma za Vivuko kutoka  wakala wa Ufundi wa umeme Tanzania Mhandisi Japhet Maselle.

Aidha, alitaja   sababu za uharibifu wa vivuko hivyo kuwa ni pamoja na baadhi ya abiria kutofuata taratibu za vivuko na wananchi kutumia mitumbwi ambayo si salama kuvukia hasa maeneo ya magogoni Dar es salaam na  Pangani Tanga .

“Utegaji wa nyavu husababisha kunasa kwenye mifumo ya kuendeshea vivuko, na takataka kuingia kwenye mitambo ya kuendeshea vivuko ambapo  husababisha athari katika mitambo hiyo” alisema ndugu Maselle.

Katika kukabiliana na matatizo hayo, TAMESA imeendelea kutoa elimu kwa watu wanaochafua mazingira na maeneo ya vivuko kutangaza taratibu za vivuko ndani ya vivuko  na kuboresha huduma za  vivuko na kuongeza maeneo yenye uhitaji.

Wakala wa ufundi na Umeme Tanzania (TAMESA) ilianzishwa kwa sheria ya wakala namba 30 ya mwaka 1997 ikiwa na lengo la kutoa huduma katika Nyanja za uhandisi mitambo, umeme na uendeshaji wa vivuko .
 
Kwa sasa kuna vivuko 28 vinavyofanya kazi katika vituo 19 Nchini, baadhi ya vivuko hivyo ni Mv Msungwi,Mv sabasaba, Mv Sengerema,Mv mwanza, Mv ukara , Mv Nyerere na Mv Temesa.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa