Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Boniface Jacob,
amesema hawatakubali kuona Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye,
anaonewa, kunyanyaswa na kudhalilishwa kwa kutumia mwavuli wa wavamizi
wa ardhi huku kukiwa na siasa ndani yake.
Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake jijini Dar es
Salaam, alisema kinachoendelea katika shamba la Sumaye ni kutengeneza
wavamizi na kwenda kuzungumza nao kuonyesha kuwa suala hilo
linashughulikiwa kwa mujibu wa taratibu.
“Hakuna mahali kokote unaweza kuendesha kesi baina ya wavamizi na
mmiliki halali, mwenye mamlaka na ardhi ni Baraza la Madiwani, vyombo
vingine ni kulinda amani na mmiliki halali anajulikana, tunachokiona kwa
sasa ni kutengeneza jambo na kutafuta ‘kiki’ ya kisiasa,” alisema na
kuongeza:
“Kama inafanyika hivi, watambue kuwa nasi tunawafahamu vigogo wa
CCM walioshikilia maeneo makubwa na hawajaendelezwa, na pembeni ya eneo
la Sumaye kuna eneo la Chuo cha IFM hilo halijavamiwa...sitakubali
kuona mwananchi wangu au kada wetu ananyanyaswa, tutamtetea kwa mujibu
wa sheria.”
Alisema manispaa hiyo iliwahi kuendesha operesheni ya kubomoa
nyumba za wavamizi 350 kwa kushirikiana na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya,
Jordan Rugimbana, lakini kwa uongozi wa wilaya wa sasa, wavamazi
wanatambuliwa na kusikilizwa.
“Wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka jana kulikuwa na vitisho kwa
madaka wa CCM waliohama chama, kinachoonekana ni utekelezaji wa uonevu.
Hawana mamlaka ya kujadili suala hilo, ni siasa zenye lengo la
kumnyanyasa kada wetu, wamefanya kosa la jinai, lazima wachukuliwe hatua
na siyo kuwekwa kikao,”alisisitiza.
Alisema uvamizi wa ardhi umekithiri katika Kata za Bunju, Wazo, Mabwepande, Bweni na Kawe.
Alisema inashangaza kuona makada wa CCM wanalibeba suala hilo kwa
mwavuli wa serikali huku ndani yake wakifanya siasa na kutafuta umaarufu
na kwamba uonevu na unyanyasaji wowote haukubaliki katika manispaa
hiyo.
Shamba la Sumaye lenye ukubwa kwa heka 33 lilivamiwa mwishoni mwa
mwaka jana, na watu ambao walijigawia viwanja na kuanza ujenzi.
Hivi karibuni, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda,
alitembelea shamba hilo akiwa na Sumaye na polisi na kuwataka wavamizi
hao kusitisha ujenzi huo haraka hadi watakapokagua vibali vya umiliki
wake.
Katika hatua nyingine alisema mipango aliyoanza nayo kuwa ni
kusafisha jiji kwa kununua magari 40 ya kuzoa taka na ya kuzishindilia
na kwamba baada ya mwaka mmoja tani 2,026 za taka zinazozalishwa kila
siku zitazolewa.
Kuhusu makusanyo ya mapato alisema atahakikisha yanafika Sh. bilioni 100 kutoka Sh. bilioni 51 za mwaka 2015/16.
Aidha, alisema Manispaa hiyo haitafanya kazi na wakandarasi
walioshindwa kutekeleza ujenzi wa miundombinu kwa viwango na kwamba
wataandika barua kwenda kwa mammlaka zote kuhakikisha hawapewi kazi
kwingine baada ya kuharibu.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment