Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mhe. Balozi Dkt. Agustino Maige
Serikali
ya Tanzania imesema kuwa inaendelea kufatilia ili kuchukua hatua zaidi
juu ya matukio yalitokea nchini India katika chuo cha Acharya Bangalore,
ikiwemo la mwanafunzi wa Kike kudhalilishwa kwa kuvuliwa nguo.
Akitoa
tamko la Serikali leo Bunge Mjini Dodoma, Waziri wa Mambo ya Nchi za
Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt.
Agustino Maige amesema tayari serikali imeshapeleka dokezi la
kidiplomasia kwa serikali ya india ili kuonyesha kukasirishwa na kitendo
hicho.
Balozi
Maige ameongeza kuwa tayari wameitaka serikali ya India kuchukua hatua
za kipolisi kufanya uchunguzi juu ya tukio hilo ikiwa ni pamoja na
kupeleka ulinzi wa kutosha katika maeneo wanaoishi wanafunzi hususani wa
kitanzania ambapo leo kumeri kwa mtu anaesadikiwa kuwa mtanzania
kufariki katika mazingira ya kutatanisha.
Kwa
upande wa baadhi ya wabunge wameiomba serikali kuwa na tamko rasmi la
kuonyesha kuchukizwa na ubaguzi kwa watanzania pindi waendapo kuishi nje
ya Tanzania.
Tukio
hilo limekuja baada ya Gazeti la Deccan Chronical la Bangalore kuripoti
kuwa tukio hilo limetokea baada ya mwanafunzi raia wa Sudan, Ismail
Mohammed kugonga gari la raia mmoja wa india mkazi wa Hessaraghata
aliekuwa na Mkewe na kusababisha kifo cha mama huyo.
Wakati
huo huo Wanaume wanne wanaotuhumiwa kuhusika katika kumshambulia na
kumvua nguo mwanafunzi wa kike kutoka Tanzania wamekamatwa, shirika la
habari la AP limeripoti.
Waziri
wa mashauri ya kigeni wa India Sushma Swaraj, aliandika kwenye Twitter
kwamba amesikitishwa sana na “kisa hicho cha aibu” kilichotokea Jumapili
eneo la Bangalore.
Source:EATV
0 comments:
Post a Comment