Na Daudi Manongi,MAELEZO.
SHIRIKA la Maendeleo
ya Petroli Nchini (TPDC) limekabidhi msaada wa Viti 142 kwa shule ya Sekondari
Kisungu iliyopo Tabata Kinyerezi Jijini Dar es Salaam.
Akikabidhi msaada huo
leo Jijini Dar es Salaam Meneja Mawasiliano wa TPDC alisema taasisi hiyo
imeamua kuunga mkono jitihada za
Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli za kupunguza uhaba wa madawati katika shule za Msingi na Sekondari
nchini.
“TPDC inaunga mkono
jitihada za Rais John Pombe Magufuli katika kumaliza tatizo la wanafunzi kukaa
chini, tumeamua kutekeleza kwa vitendo jitihada hizo” alieleza Msellemu.
Aidha Msellemu alisema
kwa kipindi kirefu TPDC imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia huduma za
kijamii nchini ikiwemo elimu na afya, ambapo hivi karibuni taasisi hiyo
ilijenga zahanati pamoja na kukabidhi Madawati 500 katika kata ya Madimba
iliyopo Mkoani Mtwara.
Akipokea msaada wa
viti hivyo, Mkuu wa Shule ya Sekondari Kisungu, Mkamo Mgeta aliishukuru TPDC
kwa msaada ambao umelenga kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri wa Muungano
wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli na kuwataka wadau zaidi kujitokeza kusaidia
uhaba huo.
MWISHO.
0 comments:
Post a Comment