WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI
TAARIFA KWA UMMA
Wizara
ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inawatangazia wananchi wote
ambao Hatimiliki zao waliziwasilisha kwa ajili ya usajili, zipo tayari
na sasa wafike kituo cha Huduma kwa Mteja ofisi ya Kamishna Msaidizi wa
Ardhi kanda ya Dar es salaam kuchukua Hatimiliki zao.
Orodha ya wamiliki hao inapatikana kwenye tovuti ya Wizara www.ardhi.go.tz na
kwenye ofisi za Idara ya Ardhi za Halmashauri za Manispaa ya Temeke,
Ilala, Kinondoni, Kisarawe, Mkuranga, Bagamoyo na Kibaha.
Mara tu uonapo jina lako katika orodha hiyo, Tafadhali fika na kitambulisho chako.
Imetolewa na:
WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI
0 comments:
Post a Comment