Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili kwa ajili ya kumpokea Mgeni wake Mfalme Mohamedi wa Sita wa Morocco leo Ikulu Jijini Dar es Salaam |
Mfalme
Mohamedi wa Sita wa Morocco Akisalimiana na baadhi ya wananchi waliojitokeza
kumpokea leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
|
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Mgeni wake Mfalme Mohamedi wa Sita wa
Morocco wakiwaangalia wapigaji ngoma mara baada ya kuwasili Leo Ikulu Jijiji
Dar es Salaam.
|
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Mgeni wake Mfalme Mohamedi wa Sita wa Morocco wakipiga ngoma mara baada ya kuwasili Leo Ikulu Jijiji Dar es Salaam. |
Baadhi
ya Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waliohudhuria hafla
ya utiaji saini wa mikataba 21 kati ya Tanzania na Morocco.
|
Waziri
wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Augustino Mahiga
akiizungumzia mikataba 21 itakayosainiwa kati ya Tanzania na Morocco.
|
Waziri
wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage akieleza namna Tanzania
itakavyonufaika na mikataba 21 iliyosaniwa katika ya Nchi ya Morocco na
Tanzania.
|
Baadhi
ya Viongozi wa Serikali na Sekta binafsi Tanzania pamoja na wenzao wa Morocco
wakisaini na kubadilishana mikataba leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
|
Na
Daudi Manongi
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli amesema kuwa wamekubaliana
na Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco kujenga Uwanja wa Mpira wa miguu wa
kisasa mkoani Dodoma utakaogharimu dola
milioni 100.
Rais
Magufuli ameyasema hayo leo Ikulu Jijini Dar es Salaam baada ya kutiliana saini
kwa mikataba 21 ya makubaliano ya ushirikiano kati ya nchi za Tanzania na
Morocco.
“Mbali
na mikataba baina ya Tanzania na Morocco nimezungumza mambo mbalimbali na
Mfalme Mohamed wa Sita wa Morocco na nimemuomba atujengee Uwanja mkubwa wa
mpira pale Makao Makuu yetu Dodoma utakaokuwa na thamani kati ya dola milioni
80 hadi 100 na amesema ataujenga, kwa hiyo
utakuwa Uwanja mkubwa kuliko wa Dar es Salaam”. Alisema Rais Magufuli.
Mbali
na hayo Rais Magufuli amewahakikishia wafanyabiashara wa Morocco kuwa Tanzania
ni salama na inapenda kushirikiana nao, na kuwa nchi yetu iko katika mwelekeo
mzuri wa uwekezaji ambapo uchumi wa nchi yetu unategemea kukua kwa asilimia 7.2
mwishoni mwa mwaka.
Kwa
upande wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco Bw.Salahddine Mezour ameishukuru
nchi ya Tanzania kwa ushirikiano iliounyesha na kusema kuwa Morocco itaendelea
kushirikiana na Tanzania katika Nyanja mbalimbali kwa kuwa ina utulivu wa
kisiasa na icho ndo kimekuwa kivutio kikubwa katika kuwekeza kwao nchini hapa.
Mfalme
Mohamed wa Sita wa Morocco yuko nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kwa
mwaliko wa Rais, Dk John Pombe Magufuli ikiwa na lengo la kuimarisha uhusiano
uliopo baina ya nchi hizi mbili na kutiliana saini mikataba 21 ya makubaliano
ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.
0 comments:
Post a Comment