Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Mhe. Serukamba: Wadau endeleeni kutoa maoni kuhusu Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari.

Mhe. Serukamba: Wadau endeleeni kutoa maoni kuhusu Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na Mwandishi Wetu Dodoma

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Mhe. Peter Serukamba ametoa wito kwa wadau wa Habari kuendelea kutoa maoni yao kuhusu Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari kwa kamati yake.

Aliongeza kuwa kwa sasa kamati yake inaendelea na kazi ya kuujadili Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari kwa kuendelea kupitia kifungu kwa kifungu na baadae kuunganisha na maoni ya wadau ambayo hayapo kwenye Muswada huo kabla ya kuupeleka kujadiliwa Bungeni.

“Nitoe tu wito kwa wadau wa Habari kuzidi kuto maoni yao kuhusu Muswada huu kwani wao ndio wahusika wakuu wa Sheria hii ” alisisitiza Mhe. Serukamba.

Mhe. Serukamba amesisitiza kuwa wadau wa habari na wanahabari wanapaswa kufahamu kuwa Muswada huo utaleta Sheria iliyo bora kwa mufaa ya tasnia ya habari na watanzania kwa ujumla.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii inaendelea kupokea maoni kutoka kwa wadau habari  kupitia barua pepe ya cna@bunge.go.tz.

MWISHO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa