Na Beatrice Lyimo-MAELEZO
Dar es Salaam
SERIKALI
imesema hakutokuwa na matumizi mabaya ya mamlaka anayopewa Waziri
anayesimamia tasnia ya habari katika muswada wa sheria ya huduma ya
habari isipokuwa kwa masuala yatakayohatarisha usalama wa Taifa.
Imesema
Serikali haiwazuii waandishi wa habari kukosoa sera, matamko na ahadi
mbalimbali zinazotolewa na Viongozi wa kitaifa pindi wanaposhindwa
kutekeleza maagizo wanayoyatoa kwa wananchi.
Akizungumza
katika mwendelezo wa ziara yake ya kutembelea vyombo mbalimbali vya
habari leo Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Idara ya Habari
(MAELEZO), Hassan Abbas alisema muswada huo unatoa fursa kwa chombo cha
habari kupeleka malalamiko yake mahakamani pindi inapotokea
kutokubaliana na hatua itakayoweza kuchuliwa na Waziri mwenye dhamana
ya habari.
Kwa
mujibu wa Abbasi alisema yapo masuala kadhaa yanayopaswa kuchuliwa
hatua za haraka za maamuzi ikiwemo suala la uchochezi, uasi wa kikundi
fulani cha watu kinachotaka kuigombanisha Serikali na wananchi.
Aliongeza
kuwa hata katika mikataba ya kimataifa ikiwemo kifungu cha 19 mkataba
wa geneva wa mwaka 1966 umeeleza kuhusu haki ya kupata habari na taarifa
ingawa upo ukomo katika masuala kadhaa ikiwemo suala la usalama wa
taifa.
“Uchochezi
ni kuhatarisha amani ya nchi, lakini mwandishi akiikosoa Serikali
haitokuwa uchochezi bali kwa atakayeleta habari za uchochezi kwa maana
ya uasi atatakiwa kuwajibishwa” alifafanua Mkurugenzi Abbas.
Aidha
alisema kuwa muswada huo umekusudia kuanzishwa kwa Baraza la Maadili
litakalokuwa na wajumbe saba, ambapo wanne kati yao ni kutoka katika
tasnia ya habari ikiwemo mwenyekiti wa Baraza na watakuwa na mamlaka ya
kusimamia maslahi na usalama wa waandishi.
Akifafanua
zaidi alisema kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa mchakato wa
kupata Sheria ya huduma ya habari unafika mwisho ambapo mchakato wake
umechukua miaka 20 mpaka sasa.
Alisema
kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa muswada huo unapitishwa na
Bunge ili uweze kuwa sheria kamili na hatimaye kuifanya tansia ya habari
kuwa taaluma yenye kuheshimika zaidi.
Pia
alisema kuwa muswada huo utasaidia sekta ya habari kuwa muhimili wenye
nguvu na taaluma iliyokamilika yenye haki zake kama upatikaji wa bima za
afya kwa waandishi wa habari.
Abbasi
alisema iwapo sheria hiyo itapitishwa itatumika upande wa Tanzania Bara
pekee na si Zanzibar, kwa kuwa suala la habari halipo katika mambo ya
Muungano, ingawa sekta hizo zinashirikiana kwa namna moja au nyingine.
0 comments:
Post a Comment