Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na
Lorietha Laurence-WHUSM
Mnamo
tarehe 16 Septemba mwaka huu Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo iliwasilisha kwa mara ya kwanza Muswada wa Sheria ya Huduma za
Habari Bungeni Mjini Dodoma.
Tangu
kuwasilishwa kwa Muswada huo kumekuwa na maoni mbalimbali kutoka kwa wadau
habari ni kwa namna gani jamii na tasnia
ya habari na itanufaika na Sheria hiyo.
Mmoja
wa wadau wa habari Bw. Malekela Maingu katika mahojiano maalum na mwandishi wa
habari hii alihoji endapo Muswada huu upo kwa ajili ya kunufaisha wanahabari
peke yake, swali ambalo wadau wengi watakuwa wakijiuliza.
Muswada
wa Sheria ya Huduma za Habari upo kwa ajili ya watu wote kwa kuwa katika Muswada
huo umezingatia kumlinda mwandishi na mwananchi kwa kutoa habari za uhakika ili
kuzuia mgawanyiko kwa jamii endapo itatokea kashfa.
Katika
sehemu ya Tano kifungu cha 32(1) cha Sheria hii inaeleza kuwa jambo lolote kama
likichapishwa au kutangazwa linaweza
kuharibu sifa ya mtu kwa kumfanya achukiwe, adharauliwe au afanyiwe kejeli au linaweza kumharibia mtu kazi yake kwa kuchafua jina lake au kumvunjia heshima yake jambo hili
litahesabika kuwa ni kashfa.
Kufuatia
kifungu hicho ni wazi Sheria hii itasimamia haki ya mtu endapo taarifa
zitakazotolewa kuhusu mtu huyo zitabainika
kuwa ni za uongo zenye nia ya kumchafulia jina ama kumdhalilisha.
Kifungo
hicho kinaendelea kueleza kuwa Sheria
hii inamtaka mwandishi wa habari kuzingatia
maadili ya uandishi kwa kutoa taarifa zilizo za kweli na zenye uhakika ili
kulinda maslahi ya nchi na watu wake.
Naye
Bw. Amour Kagya ameipongeza Serikali kwa kuleta Muswada wa Sheria ya Huduma za
Habari na kueleza kuwa kupitia Sheria hii kazi ya uandishi wa habari
itaheshimiwa na kuthamaniwa.
Bw.
Kagya amesema wanahabari watanufaika kwa uwepo wa mfuko wa mafunzo ya habari kwani
utawasaidia kujiendeleza na kukuza tasnia ya uandishi wa habari hivyo kuipa
hadhi fani hiyo.
Mwisho.
0 comments:
Post a Comment