Kampuni ya ndege Tanzania (ATCL) inapenda kutoa taarifa kwa
umma kuwa kwa sasa ina ndege tatu,
zikiwemo mbili mpya aina ya Dash8-Q400
zenye uwezo wa kubeba abira 76 kila moja na Dash8-Q300 moja yenye uwezo wa kubeba abiria 50.
Ndege hizo zinaendelea kufanyiwa ukaguzi na mamlaka ya
usafiri wa anga (TCAA). Zoezi hilo litakapokamilika kutakuwa na mazoezi ya
vitendo kwa marubani na wafanyakazi wengine wa ndani ya ndege. Safari za
biashara za kuruka na abiria zinatarajiwa kuanza tarehe 15 Oktoba 2016 na zitafanyika
kwenye viwanja vifuatavyo:- Mwanza, Arusha, Zanzibar, Kigoma, Tabora, Mbeya,
Mtwara, Kilimanjaro, Bukoba, Dodoma na Mpanda - nchini. Nje ya nchi yetu ATCL
itaruka kwenda Comoro, Nairobi na Entebbe.
Aidha, ATCL inachukua fursa hii kuwaomba wadau wake wote kuwa
na subira wakati tukiendelea kusubiri taratibu za mamlaka ya usafiri wa anga
zikamilike.
Imetolewa na;
KAIMU MKURUGENZI
MTENDAJI
AIR TANZANIA
0 comments:
Post a Comment