Na Godfriend Mbuya
Jeshi la polisi nchini limesema halipendelei chama chochote
cha siasa nchini na badala yake linachofanya ni kutoa ulinzi wa kuhakikisha
mali na usalama wa raia upo wakati wote.
Hayo yamesemwa na Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania ACP
Advera Bulimba wakati akizungumza na wananchi waliokuwa wakimuuliza maswali
katika kipengele cha KIKAANGONI
kinachorushwa kupitia ukurasa wa facebook wa EATV ambapo baadhi ya
wananchi walitoa madukuduku yao kuhusu upendeleo kwa baadhi ya vyama vya siasa nchini.
“ Jeshi la polisi halina upendeleo kwa chama chochote cha
siasa nchini, ndiyo maana kila chama kikizingatia kanuni za kuomba mikutano ya
hadhara kinapata ulizi kutoka jeshi la polisi, hivyo kazi yetu kubwa ni
kuhakikisha usalama wa raia na mali zao upo hivyo tukizuia mkutano wowote ni
kwea lengo la kudumisha usalama wa raia na mali zao na kupafanya Tanzania kuwa
sehemu salama ya nchi.
Aidha Jeshi la polisi limewataka wananchi kuendelea kutoa
taarifa ambazo zitasaidia kuimarisha ulinzi na usalama na taarifa watakazotoa
zitachukuliwa maanani na kufanyiwa kazi mara moja, na namba za kutumika ni 111
au 112.
0 comments:
Post a Comment