Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Immaculata Makilika- MAELEZO
Moroko ni
nchi iliyopo Kaskazini Magharibi mwa Afrika, ambayo imepakana na bahari za Atlantiki
na Mediteraniani, na upande wa bara imepakana na nchi za Algeria, Mauritania.mpaka
wa kusini unatajwa kuwa Sahara Magharibi.
Nchi ya Moroko inakadiriwa kuwa na eneo la Km2 446,550, huku sehemu kubwa
ikiwa ni jangwa la Sahara na watu wengi nchini humo huishi kwenye sehemu zilizo
na rutuba hasa karibu na maeneo ya pwani.
Nchi hiyo ina milima inayofunika eneo kubwa, ikiwemo milima ya Atlas ambayo
ipo katikati ya nchi hiyo kutoka kusini magharibi kuelekea upande wa kaskazini
mashariki na mji mkuu wake ukiwa ni Rabat wenye wakazi milioni 2, aidha mji
mkubwa ni Casablanka.
Nchi ya Moroko
ilipata uhuru wake mwaka 1956 kutoka kwa nchi za Ufaransa na Hispania
zilizokuwa zikiitawala, na kikatiba inaongozwa
na Mfalme, kwa sasa inaongozwa na mfalme
anayeitwa Mohammed wa VI, na Waziri Mkuu
ni Abdelilah
Benkirane.
Watu wa Moroko
hutumia lugha rasmi za kiarabu na
kiberiberi. Fedha yao inajulikana kama Dirham, zaidi ya 90% ya watu wake ni waislamu.
Uchumi wa Moroko
unategemea zaidi utalii, sekta ya mawasiliano, viwanda vya nguo pamoja na
kilimo.
Hivi
karibuni, kwa mara ya kwanza
tunashuhudia ziara ya Mfalme wa Moroko Mohammed wa VI aliyewasili nchini wiki
hii kwa ziara ya siku tatu hadi Oktoba 25 mwaka huu.
Ujio wa Mfalme
huyo wa Moroko unaidhihirishia dunia kwa
kiasi gani diplomasia ya Tanzania imeendelea kukua kwa kasi, ikiwa ni sambamba
na kukuza diplomasia ya uchumi.
Waziri wa Mambo
ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Augustine Mahiga anasema kuwa lengo la ziara
hiyo ni kukuza uhusiano wa kati ya Tanzania na Moroko hususani katika masuala
ya uchumi na biashara kwa faida ya watu wa nchi hizi mbili.
“ Ziara hii
imejikita zaidi katika kukuza ushirikiano wa kiuchumi na biashara, ikizingatiwa
kuwa nchi ya Moroko imefanikiwa katika nyanja mbalimbali kama vile miundombinu,
afya, madini na ulinzi”.
“Vile vile wafanyabiashara kutoka Moroko watafanya
mazungumzo na wa hapa nchini kwa lengo la
kubadilishana uzoefu na ni hatua nzuri itakayoweza itakuza uhusiano wetu pamoja
na kuchochea maendeleo ya kiuchumi” anasema Balozi Mahiga.
Maroko imepiga
hatua katika sekta mbalimbali ikiwemo utalii, uvuvi ,viwanda, kilimo na madini.
Mambo yaliyopo
katika mpango huo ni pamoja na maboresho ya reli, na barabara, kuboresha
viwanja vya ndege kwa viwango vya kimataifa ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi
ya ndege zinazoingia Moroko. Sambamba na hilo bandari maarufu zimeandaa
utaratibu wa safari za kitalii.
Vitu na Maeneo
mbalimbali yamekuwa sehemu ya kuvutia utalii kutoka nchi za Ujerumani, Ufaransa,
na Hispania, ambapo huvutiwa na fukwe za
bahari,milima ya Atlas, pamoja na miji maarufu ya kama ya Tangie, Marrakech,
Casablanka na Tarfaya.
Sekta ya madini
ni sekta muhimu kwa vile inachangia uchumi wa nchi kwa asilimia 6 ya pato la ndani la taifa na asilimia 35 ya pato la kigeni kwa nchi ya Moroko.
Ili kukuza sekta
ya utalii nchini humo, matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA)
yameimarishwa na kuweza kutangaza
vivutio mbalimbali kwa kuhususha sekta binafsi katika kutangaza utalii wa
ndani, na kati ya nchi zilizofanikiwa katika hilo ni pamoja na nchi ya Malaysia
ambapo mwaka 2011 ilipata watalii milioni 24.7 na mwaka 2012 ilipata watalii
milioni 25 kutokana na matumizi ya TEHAMA.
Jitihada
mbalimbali zimefanyika katika kusaidia
sekta ya utalii nchini kukua na kuchangia zaidi pato la taifa, ambapo kupitia maboresho
kuongeza ndege zenye safari ya moja kwa moja hadi nchini, na kuboresha
miundombinu ya barabara sekta hiyo imeweza kupata mafanikio.
Gavana wa Benki
Kuu ya Tanzania, Prof. Benno Ndulu anasema kuwa
hivi sasa sekta ya utalii inakuwa, ambapo imechangia zaidi katika pato
la ndani la taifa mara tatu kuliko sekta ya kilimo iliyokuwa ikichangia zaidi
uchumi wa nchi.
“Sasa sekta ya utalii
inakusanya dola bilioni 1 fedha ambazo ni
mara tatu zaidi ya sekta ya kilimo, sekta ambayo kwa miaka mingi ilikua
ikichangia kwa kiasi kikubwa katika pato la ndani la taifa” anasema Prof.
Ndulu.
Kufuatia
jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali katika kukuza uchumi wa nchi,
ziara hii ni fursa ya kipekee kwa serikali pamoja na wafanyabiashara wa
Tanzania kwa kujifunza kutoka kwa wataalamu mbalimbali wa nchini Moroko kwa
lengo la kukuza pato na hatimaye uchumi wa nchi.
mwisho
0 comments:
Post a Comment