Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Watumishi wa Umma waaswa kuzingatia maadili

Watumishi wa Umma waaswa kuzingatia maadili

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Frank Mvungi-Maelezo
Watumishi wa Umma wametakiwa kuzingatia maadili na kuacha kutumia madaraka yao vibaya kwa maslahi binafsi hali inayoweza kuzorotesha huduma wanazotoa kwa wananchi.
Onyo hilo limetolewa na Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Kinondoni Bw. Benn Lincoln kufuatia kukamatwa kwa Afisa Afya wa Kata ya Mbweni Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam Bw. Amos Ndalawa kwa makosa ya kuomba na kupokea rushwa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TAKUKURU, mshtakiwa huyo alifikishwa kwenye Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni na kufunguliwa mashtaka mawili ya kuomba na kupokea rushwa kinyume na kifungu namba 15(1)(a) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007.
Mwendesha mashitaka wa TAKUKURU Bibi. Vera Ndeoya aliieleza Mahakama kuwa mshitakiwa akiwa mwajiriwa wa Halmashauri ya Kinondoni kama Afisa Afya wa Kata ya Mbweni mnamo tarehe 21 Machi, 2017 alishawishi na kupokea rushwa ya shilingi laki 3 kutoka kwa Leticia Lubala ili asimchukulie hatua za kisheria baada ya kukagua biashara yake. Ilisisitiza sehemu ya taarifa hiyo.
Taarifa hiyo iliongeza kuwa kesi hiyo imeahirishwa hadi Aprili 10 mwaka huu kwa vile uchunguzi haujakamilika.

 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa