Mkurugenzi Mkazi wa Asasi ya Kiraia ya Global Peace Foundation(GPF) nchini Tanzania Bi. Martha Nghambi akielezea shughuli za asasi hiyo na nafasi ya mwanamke katika uongozi.
Baadhi ya washiriki katika Kongamano hilo la Mwanamke na uongozi wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkazi wa Asasi ya Kiraia ya Global Peace Foundation(GPF) nchini Tanzania Bi. Martha Nghambi ambaye (hayupo pichani)
Aliyekuwa Mgeni Rasmi katika kongamano hilo lililo andaliwa na Makamu wa Rais wa serikali ya wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es salaam(DARUSO) Bi. Shamira Mshangama Mh. Sophia Mjema akitoa nasaha zake kwa wote waliohudhuria katika kongamano hilo.
Makamu wa Rais wa Serikali ya wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es salaam Bi. Shamira Mshangama akieleza kwa ufupi juu ya Kongamano hilo na Kumkaribisha Mkurugenzi wa Maswala ya Jinsia Chuo Kikuu Cha Dar es salaam Dkt. Kafanabo
Mkurugenzi wa Maswala ya Jinsia Chuo Kikuu Cha Dar es salaam Dkt. Kafanabo akielezea kwa undani juu ya jinsia na uongozi katika kongamano hilo
Meneja wa Benki ya NMB PLC tawi la Chuo Kikuu cha Dar es salalaam Bi. Rehema Mwibura akielezea safari yake ya uongozi mpaka hapa alipofikia sasa na kuwaatha vijana wakike wasikate tamaa kwa kuwa wanaweza.
Mwanachama wa zamani wa USRC Bi. Yunge Kanuda akiwasihi vijana wanawake kuwa wanayo nafasi ya kugombea ngazi mbalimbali za uongozi hivyo wanatakiwa wathubutu ili waweze kushika nyadhifa mbalimbali.
Washiriki wa Kongamano hilo wakifuatilia kwa makini mijadala mbalimbali inayoendelea
Mkurugenzi Mkazi wa GPF Bi Martha Nghambi(Kulia) akifuatilia mada mbalimbali wakati wa Kongamano hilo
Mkurugenzi Mkazi wa GPF Bi Martha Nghambi(Kulia) akifuatilia mada mbalimbali wakati wa Kongamano hilo
Aliyekuwa Spika wa Bunge la USRC kwa mwaka 2014/2015 Protus Petro akielezea juu ya uongozi
Aliyekuwa Makamu wa Rais wa Serikali ya wanafunzi Chuo Kikuu cha Dar es salaam Irene Ishengoma na aliyeshiriki Shindano la Maisha Plus 2016 akielezea mambo mbalimbali yanayowahusu wanawake na kuwasihi kuto bweteka kwa kuwa wanaweza.
Baadhi ya Washiriki wa Kongamano hilo wakiuliza maswali na kuchangia mawazo katika Kongamano hilo.
Mwanzilishi
na Rais wa Taasisi ya wanafunzi wanawake kutoka Chuo Kikuu cha Dar es
salaam Consolata Chikoti akifuatilia kwa makini mijadala ikiendelea.
Washiriki katika Kongamano hilo
Picha zote na Fredy Njeje
Na Dickson Mulashani
Makamu wa Rais wa
Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Bi. Shamira Mshangama kwa
kushirikiana na Asasi ya Kiraia ya Global Peace Foundation(GPF) Tanzania na
wadau wengine aliandaa kongamano kwa ajili ya Mwanamke na Uongozi likiwa na
lengo la kuwafanya wanawake wapate kutambua kuwa wanaweza kuwa viongozi katika
ngazi mbalimbali bila kuwa na uoga wowote
Akizungumza
katika Kongamano hilo Mkurugenzi mkazi wa Asasi ya kiraia ya Global Peace
Foundation (GPF) Martha Nghambi alielezea kwa undani kuwa " GPF ni ni
Taasisi isiyo ya kiserikali,ambayo si ya kidini na haitengenezi faida ya aina
yoyote ile ina makao yake makuu katika jiji la Washington DC nchini
Marekani na lenye matawi yapatayo 23 duniani kote, yakiwemo mabara ya
Afrika,Ulaya, Asia na Marekani ni “Taasisi hii kwa Tanzania ilianzishwa kati
kati ya Mwaka juzi 2015 ambapo pamoja na uchaga wake wameonesha juhudi kubwa
katika kuhamasisha amani nchini kuanzia ngazi ya familia na jamii kwa
ujumla."
Pia Mkurugenzi huyo
akiongelea umuhimu wa wanawake katika nafasi mbalimbali za uongozi aliwasihi
vijana wakike tangu wakiwa wadogo wawe na watu ambao ndio mfano kwao "Role
Model" watakao wafanya kutimiza ndoto zao, pia kuwa na uthubutu kwa kuwa
wanaweza kushika nyadhifa mbalimbali kuanzia ngazi ya chini mpaka uongozi wa
juu.
Nae Mkuu wa
Wilaya ya Ilala Mh. Sophia Mjema ambaye alikuwa mgeni Rasmi katika Kongamano
hilo aliwaeleza washiriki wa kongamano hilo safari nzima ya maisha yake katika
uongozi lengo likiwa kuwapa mwanga kuwa wanawake wanaweza kushika nafasi
mbalimbali bila wasiwasi.
Mh. Sophia Mjema
aliwaatha vijana hasa wa vyuoni na mashuleni kuto danganyika na kutoa rushwa ya
ngono na kuto kujirahisiha maeneo ya kazi ili mtu fulani ampende amchukue ili
apate kitu fulani na kusisitiza kuwa hayo ni mambo yanapita na waepuke tamaa
hizo.
Aliongeza kuwa
kwa wanawake wote ambao wanania ya kugombea nafasi kama Ubunge pindi wanapopata
wawe mbele zaidi katika kutetea maslahi ya wanawake kwa kuwa wao wanaona mambo
mengi zaidi katika jamii
Mwisho
alisisitiza kuwa mambo yote yanawezekana endapo amani itadumishwa katika eneo
la kazi kwa kuwa sehemu ambayo haina amani hata utendaji wa kazi huwa ni mgumu,
alisema kuwa watu wakipendana na swala zima la kazi litakuwa na ufanisi zaidi.
0 comments:
Post a Comment