Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imedhamiria kusaidia azma ya serikali katika kujenga Tanzania ya viwanda kwa kusaidia upatikanaji wa mali ghafi kwa viwanda nchini kwa kutoa mikopo nafuu kwa wakulima nchini.
Azma hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TADB, Bibi Rosebud Kurwijila wakati wa utiaji saini Mkataba wa Makubaliano ya Utekelezaji wa Mkakati wa mwaka kati ya Msajili wa Hazina na Benki hiyo katika hafla iliyofanyika Ofini kwa Msajili wa Hazina jijini Dar es Salaam.
Bibi Kurwijila amesema kwamba TADB itakeleza kwa vitendo juhudi
za Serikali za Kujenga Uchumi wa Viwanda kwa kuhuisha uwekezaji kwenye
Viwanda vidogo vidogo na vya kati vya usindikaji na uchakataji wa mazao
ya Kilimo, mifugo, samaki na misitu ili kuongeza tija ya kilimo hivyo
kutoa malighafi kwa viwanda nchini.
“Benki
imepitia upya mpango mkakati wake katika kutoa mikopo ili kuwezesha
kufikia wakopaji wengi zaidi ili kuweza kufikia lengo la kuleta
maendeleo katika sekta ya kilimo hasa katika kuongeza tija ya kilimo
hivyo kutoa malighafi kwa viwanda nchini,” alisema Bibi Kurwijila.
Bibi
Kurwijila ameongeza kuwa katika kuchagiza malengo hayo, TADB imejpanga
katika Kushirikiana na wadau mbalimbali kufanya upembuzi wa miradi ya
Maendeleo ya Kilimo na Umwagiliaji nchi nzima ili kubaini mahitaji
halisi ya fedha na pia kusaidi kupanga maeneo ya vipaumbele ili kuanza
kutoa mikopo hasa kwa utaratibu mahsusi.
Ametaja
malengo mengine ya kimkakati ya TADB ni pamoja na kuboresha huduma kwa
kuanzisha mazao maalum ya huduma za kibenki kwa wakulima wadogowadogo
kulingana na mnyororo husika wa thamani na pia kuanza huduma za Zaidi
kupitia taasisi za fedha zilizopo (wholesale lending and Refinancing)
ili kufikia wakulima wengi zaidi.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga amesema kuwa mpaka sasa Benki imefanikiwa kukopesha jumla ya shilling bilioni 6.5 kwa vikundi 20 vyenye jumla ya wakulima 2575.
Bw.
Assenga ameongeza kuwa Benki imeweza kuvijengea uwezo vikundi 336 vya
wakulima wadogowadogo vyenye jumla wa wanachama 44,400 katika mikoa ya
Iringa, Morogoro na Tanga.
“Kupitia
mafunzo hayo TADB imewezesha jumla ya vikundi 19 kutimiza masharti na
maandalizi ya msingi ya kuweza kukopa; Vikundi vingine vilivyobaki
vinaendelea kupatiwa mafunzo ili viweze kufikia hali ya kuweza
kukopesheka,” ameongeza.
Kwa
mujibu wa Bw. Assenga, TADB imeweza kuinua idadi ya wakulima watumiao
mabenki na vyombo vya fedha wapatao 2,359 ambao kati yao wanawake ni 863
sawa na asilimia 36.6 ya wanufaika.
Akizungumza
wakati wa hafla hiyo, Msajili wa Hazina, Dk. Oswald Mashindano alisema
taasisi za umma zina wajibu wa kuisaidia utekelezaji wa mipango
mbalimbali ya Serikali ili kuleta maendeleo endelevu nchini.
0 comments:
Post a Comment