Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » SIKU YA KUCHANGIA DAMU DUNIANI, MSAADA WA PICHA NA STORY-MUHIMBILI

SIKU YA KUCHANGIA DAMU DUNIANI, MSAADA WA PICHA NA STORY-MUHIMBILI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

unnamed
Mkuu wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, Mheshimiwa Sophia Njema akizungumza na Jonas Hans Atile (kushoto) ambaye amejitokeza kuchangia Damu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Leo.
1
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Shirikishi Katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dk. Praxeda Ogweyo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Siku ya Kuchangia Damu Duniani. Pia Dk. Ogweyo amewataka Watanzania wajitokeze kwa wingi kuchangia damu.
2
Mmoja wa Wananchi akishiriki katika maadhimisho ya Siku ya Uchangiaji Damu duniani Leo katika hospitali hiyo.
3
Baadhi ya wananchi wakisubiri kuchangia damu Leo katika jengo la Maabara kuu, hospitali ya Taifa Muhimbili
4
Baadhi ya Wananchi waliojitokeza kuchangia damu katika Hospitali ya Muhimbili wakiendelea na shughuli ya utoaji damu Leo.
……………………………….
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo imeshiriki katika madhimisho ya Siku ya Kuchangia Damu duniani kwa kuendesha shughuli ya utoaji damu kwa watu mbalimbali ili kukidhi mahitaji ya huduma hiyo kwa wagonjwa wenye uhitaji.
Shughuli hiyo inaendelea katika hospitali hiyo kwenye Jengo la Maabara kuu ambako watu wamekusanyika kwa ajili ya kuchangia damu. Mmoja wa viongozi walishriki katika maadhimisho hayo ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam, Mheshimiwa Sophia Mjema pamoja na Watanzania mbalimbali.
Akizungumza katika shughuli hiyo Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi kuchangia damu ili kuokoa maisha ya wagonjwa wanaohitaji huduma hiyo wakiwamo kinamama na watoto wadogo.
“Nawapongeza wote walifika leo hapa Hospitali ya Muhimbili kuchangia damu, ni jambo la muhimu mmefanya kwa ajili ya kuokoa maisha ya wagonjwa,” amesema Mheshimiwa Mjema.
Naye Mkurugenzi wa Huduma za Tiba Shirikishi wa hospitali hiyo, Dk Praxeda Ogweyo amewataka wananchi,mashirika  ya umma na yasiyo ya kiserikali, shule, vyuo mbalimbali na taasisi za dini  kujitokeza kuchangia damu hospitali hapo.
Dk Ogweyo amesema kuwa Muhimbili inahitaji wastani wa chupa za damu 100 hadi 120 kwa siku na kwamba damu inayokusanywa ni kati ya chupa 50 hadi 60 na upungufu wa damu ni chupa 60 hadi  hadi 70, hivyo damu inahitajika zaidi.
“Kutokana na hali hii, naomba rai kwa wananchi kujitokeza kwa wingi ili kuokoa maisha ya wagonjwa. Hospitali imejipanga kupitia kitengo chake cha uchangiaji damu kilichopo maabara kuu hivyo karibuni mchangie damu,” amesema Dk Ogweyo.
PICHA NA  JOHN STEPHEN, HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa