Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Wataalamu wasisitiza mazingira safi, lishe bora

Wataalamu wasisitiza mazingira safi, lishe bora

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Mratibu wa kampeni ya kitaifa Bw. Anyitike Mwakitalima akizungumza wakati wa mkutano kujadili uhusiano kati ya usafi wa mazingira na lishe bora kwa watoto jijini Dar es Salaam juzi.
 Dkt Generose Mulokozi (kulia) kutoka shirika la IMA World Health akisema ‘Nipo Tayari’ kuunga mkono kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira kwa lengo la kuzuia magonjwa ya kuhara kama vile kipindupindu yanayogharimu maisha ya Watanzania.
Mtaalamu wa lishe wa Unicef Mauro Brero akitoa ishara ya kuunga mkono kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira yenye kauli mbiu ya Nipo Tayari ikiwa na lengo la kuzuia magonjwa ya kuhara kama vile kipindupindu yanayogharimu maisha ya Watanzania.


.Washirika wa maendeleo nchini wamekutana jijini Dar es Salaam leo kujadili, pamoja na mambo mengine, umuhimu wa usafi wa mazingira katika lishe bora kwa watoto na kuunga mkono kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira yenye kauli mbiu ya “Nipo Tayari”.

Kampeni hiyo inayoratibiwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Njisia, Wazee na Watoto imejikita katika kuhamasisha watu, mijini na vijijini, kujenga utamaduni wa kuwa na vyoo na kuvitumia kikamilifu na kunawa mikono na sabuni mara baada ya kutoka chooni.

“Bila kuzingatia usafi wa mazingira, lishe bora kwa mtoto inaweza kuathiriwa na magonjwa ya kuhara kama vile kipindupindu, hivyo kuondoa virutubisho vyote mwilini. Ndio maana usafi wa mazingira na lishe bora kwa watoto ni vitu vinavyotakiwa kwenda pamoja”, anasema Dkt Generose Mulokozi kutoka shirika la IMA World Health.

Akizungumza katika mkutano huo, Mratibu wa kampeni hiyo ya kitaifa Bw. Anyitike Mwakitalima alisema: “Mazingira machafu na ukosefu wa vyoo umethibitika kuwa chanzo kikubwa kinachosababisha kudumaa kwa watoto chini ya umri wa miaka mitano. Takwimu zinaonyesha kwamba asilimia 34 ya watoto wa umri huo nchini wamedumaa kutokana na kuishi katika mazingira yasiyokuwa na vyoo na kutozingatia kanuni za afya.

Alisema kuwa ukosefu wa lise bora pia hupunguza kinga ya mwili kwa watoto hivyo kuugua mara kwa mara na kuwafanya kushindwa kukua vizuri kimwili na kiakili.

Utafiti wa afya uliofanywa nchini Tanzania 2015-16 umeonyesha mafanikio ambapo namba ya watoto waliodumaa imepungua hadi asilimia 34 ikilinganishwa na mwaka 1992 wakati nusu ya watoto walikuwa wamedumaa.

Utafiti mwingine uliofanyika nchini hivi karibuni umeonyesha kuwa madhara ya udumavu kwa watoto hauishii utotoni bali huwa na matokeo hasi kwa watu wazima na kuathiri kipato chao kwa asilimia 20. Hii inarudisha nyuma maendeleo ya nchi kwa ujumla.

Inatarajiwa kuwa asilima 75 ya Watanzania watakuwa wanaishi katika mazingira safi ifikapo mwaka 2025 na asilimia 100 mwaka 2030. Mafanikio hayo makumbwa yatafikiwa ikiwa serikali itaendelea kufanya kazi kwa karibu na washirika wa kimaendeleo wa kimataifa kufanikisha mpango huo.

Mkutano huo ulihudhuriwa na wadau wa maendeleo kutoka Action against Hunger, Aga Khan Foundation-Tanzania, Catholic Relief Services, Child Investment Fund Foundation, Department for International Development, Doctors with Africa CUAMM, Embassy of Switzerland, Feed the Children na Global Affairs Canada.

Wengine ni Global Alliance for Improved Nutrition, Ifakara Health Institute, IMA World Health, Institute of International Programs Johns Hopkins University, and International Fund for Agricultural Development, International Potato Center, United Nation Children Fund, UN World Food Program, United States Agency for International Development, World Bank, World Health Organization na World Vision International.
--

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa