Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » ADA KUBWA TLS KIKWAZO KWA MAWAKILI.

ADA KUBWA TLS KIKWAZO KWA MAWAKILI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

 Na Thobias Robert.
 Imebainika kuwa ada kubwa inayotozwa na Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS),imekuwa kikwazo kwa wanachama kujiunga hivyo kukosa haki yao msingi ya kuwa wanachama na hivyo kunyimwa haki ya kushikiri kwenye chama chao cha kitaaluma.
Hayo yamesemwa na Wakili wa Kujitegemea ambaye pia ni Mwanachama wa chama hicho, Bwana Emmanuel Makene alipokuwa akizungumza na Wandishi wa habari mapema leo Jijini Dar es Salaam kuhusu changamoto zinazoendelea ndani ya chama hicho.
“Mawakili tunatumia zaidi ya milioni 2 hadi 4 kwa mwaka kwa ajili ya malipo mbalimbali ya chama,ikiwemo ada ya uanachama, kuidhinishwa na Serikali na kuhuisha leseni ya uwakili ya kila mwaka” alisema Makene.
Aidha mawakili wanatakiwa kulipa ada ya uanachama wa Afrika Mashariki (EALS) kiasi cha dola 50 za Kimarekani kila mwaka. Malipo mengine ambayo mawakili wanapaswa kulipa ni pamoja na pesa za ujenzi wa jengo la chama (Wakili House) ambapo ndani ya chama hicho hakuna mwanachama yeyote mwenye hisa.
Pamoja na malipo makubwa ndani ya chama hicho, Makene amesema kuwa chama hakina msaada wowote kwa mwanachama endapo atapata tatizo lolote kama vile ugonjwa,jambo ambalo linawakwaza na kuhoji pesa wanachanga za nini.
“Wakili ukiwa mgonjwa au upate tatizo lolote chama hakitoi hata senti moja sasa hela tunachangia za nini ,kiufupi hatufaidiki na chama chetu japo tunalipa pesa nyingi,” alisema Wakili Makene.
Mbali na malalamiko ya kuwepo kwa michango mingi, Bwana Makene alisema kuwa, chama kina hati chafu kutoka kwa Mkaguzi wa Mahesabu ya Serikali ya mwaka 2015 ambapo chama kinatuhumiwa kwa ubadhilifu wa fedha zaidi ya milioni 200.
“Kuna tuhuma za ubadhilifu wa fedha za chama ambao umefumbiwa macho. Mkaguzi wa mahesabu alionesha ubadhilifu mkubwa na akatoa hati chafu kwa TLS mwaka 2015,ambapo taarifa ya mkaguzi wa nje wa mahesabu ya TLS ameonesha zaidi ya milioni 200 kuwa hazijulikani zilipo,” alisema wakili Makene
Pia Wakili huyo alitoa wito kwa Mawakili na wadau wa sheria kutii sheria na kujiepusha na kauli zinazoligawa taifa, “Tujitahidi sana kuchunga kauli zetu hasa kuhusiana na jamii tunayoishi ili tusiwagawe watu kidini, kikabila ama kiitikadi,na tukumbuke kuwa mawakili hatuko juu ya sheria” alisema Makene
Hayo yamesemwa na Wakili wa Kujitegemea ambaye pia ni Mwanachama wa chama hicho, Bwana Emmanuel Makene alipokuwa akizungumza na Wandishi wa habari mapema hii leo Jijini Dar es Salaam juu ya malalamiko na changamoto zinazoendelea katika chama hicho.
“Mawakili tunatumia zaidi ya milioni 2 hadi milion 4 kwa mwaka kwa kulipa kwenye chama cha mwakili. Ada ya mwananchama kwenye chama cha TLS ni kubwa sana kuliko taasisi za taaluma.
Chama cha Mawakili Tanganyika kilianzishwa kwa sheria ya Bunge ya mwaka 1954 kwa lengo la kulinda na kutetea masilahi ya mawakili Tanzania bara, kutoa elimu na msaada wa kisheria kwa wananchi lakini pia kutetea na kusimamia masilahi ya wanyonge nchini.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa