Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » BALOZI WA ISRAEL NCHINI MHE. YAHEL VILAN AWAAGA WAFANYAKAZI WA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) BAADA YA KUMALIZA MUDA WAKE WA KUFANYA KAZI HAPA NCHINI

BALOZI WA ISRAEL NCHINI MHE. YAHEL VILAN AWAAGA WAFANYAKAZI WA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) BAADA YA KUMALIZA MUDA WAKE WA KUFANYA KAZI HAPA NCHINI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimshukuru Balozi wa Israel nchini mwenye makazi yake jijini Nairobi nchini Kenya Mhe. Yahel Vilan (kulia) kutokana na nchi yake kuisaidia Taasisi hiyo kuwapatia mafunzo madaktari, wauguzi na kutoa matibabu kwa watoto. Katikati ni Daktari Bingwa wa Moyo kwa watoto na Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Moyo Sulende Kubhoja.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akizungumza na Balozi wa Israel nchini mwenye makazi yake jijini Nairobi nchini Kenya Mhe. Yahel Vilan wakati alipotembelea Taasisi hiyo leo kuwaaga wafanyakazi baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini. Israel imekuwa ikiisadia JKCI kwa kutoa mafunzo kwa madaktari, wauguzi na matibabu kwa watoto.
Balozi wa Israel nchini mwenye makazi yake jijini Nairobi nchini Kenya Mhe. Yahel Vilan akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi wakati alipotembelea Taasisi hiyo leo kuwaaga wafanyakazi baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini. Israel imekuwa ikiisadia JKCI kwa kutoa mafunzo kwa madaktari, wauguzi na matibabu kwa watoto.
Mwanamuziki kutoka nchini Israel Maestro Nir Brand akiwaimbia wimbo watoto wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakati balozi wa nchi hiyo Mhe. Yahel Vilan alipotembelea Taasisi hiyo kuwaaga wafanyakazi baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini.
Balozi wa Israel nchini ambaye makazi yake yapo Nairobi nchini Kenya Mhe. Yahel Vilan (watatu kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi pamoja wa wafanyakazi wa Taasisi hiyo na wageni kutoka nchini Israel.
Daktari Bingwa wa Moyo kwa watoto na Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Moyo Sulende Kubhoja wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) akizungumza na Daktari Bingwa wa mfumo wa chakula kwa watoto Cohen Shlomi kutoka nchini Israel wakati wa ziara ya balozi wa nchi hiyo alipotembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kuwaaga wafanyakazi.
Baadhi ya watoto wanaotiba katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiliza Balozi wa Israel nchini ambaye makazi yake yapo Nairobi nchini Kenya Mhe. Yahel Vilan alipokuwa akiwaaga wakati wa ziara yake aliyoifanya leo katika Taasisi hiyo. Serikali ya Israel kupitia Taasisi ya Save Child Heart (SACH) imegharamia matibabu ya watoto 40 tangu Novemba 2015 hadi sasa ambao walitibiwa nchini humo.
Balozi wa Israel nchini ambaye makazi yake yapo Nairobi nchini Kenya Mhe. Yahel Vilan akizungumza na wafanyakazi pamoja na watoto wanaotibiwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete wakati wa ziara yake ya kuwaaga aliyoifanya leo baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini. Israel imekuwa ikiisadia Taasisi hiyo kutoa mafunzo kwa madaktari, wauguzi na matibabu kwa watoto.

Picha na JKCI

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa