Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Bushiri Matenda na Thobias Robert-Maelezo
Chama
cha kutetea Abiria Tanzania (CHAKUA) kimemuomba Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kutoa maelekezo rasmi kwa
Mamlaka ya Usimamizi wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kuharakisha uanzishwaji wa mfumo wa ukataji tiketi kwa njia ya kielektroniki.
Mwenyekiti
wa CHAKUA Taifa, Hassan Mchajama, ametoa kauli hiyo leo, Jijini Dar es
Salaam wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu hasara inayoipata
Serikali kwa kutotumika kwa tiketi za kielektroniki kwa vyombo vya
usafiri.
Mchajama
amesema kuwa chama hicho kimekuwa mstari wa mbele kuelimisha Umma
pamoja na kuzungumza na mamlaka husika juu ya umuhimu wa kuwa na mfumo
bora wa utoaji huduma ikiwemo suala zima la ukataji wa tiketi za mabasi
kwa njia ya kielektroniki.
“CHAKUA
tunaamni kuwa suluhisho la kuwaondolea abiria kero na usumbufu wa
kuibiwa, kulanguliwa tiketi, kudhalilishwa na wapiga debe na kuuziwa
tiketi feki liko katika kuanza kwa matumizi ya mfumo wa ukataji tiketi
kwa njia ya kielektroniki,” alisisistiza Mchajama.
Kupitia
mfumo wa kielektroniki utawezesha Serikali kukusanya mapato yake kwa
uhakika kuliko ilivyo sasa na kumsaidia mtumiaji wa huduma kununua
tiketi popote alipo na kuepusha adha zinazojitokeza sasa kwa abiria.
Pia
chama hicho kimepongeza juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano katika
kuleta mabadiliko makubwa na yenye tija kwa Taifa ikiwemo kufunguliwa
kwa Kituo maalum cha kuhifadhi kumbukumbu za matumizi ya malipo na
utoaji risiti kwa mfumo wa Kielektroniki.
Aidha
Mchajama amesema kuwa, Serikali inapoteza takribani shilingi milioni
300 kila baada ya miezi mitatu kutokana na kutotumika kwa tiketi za
kielektroniki kwa wasafiri wa mabasi.
Mwenyekiti
huyo alitoa wito kwa wadau wote wanaohusika na usafirishaji wakiwemo
SUMATRA, TRA, Jeshi la Polisi, TABOA kwa pamoja waweze kushirikiana
katika kuharakisha mchakato wa uanzishwaji wa mfumo huo.
Chama
cha CHAKUA kimekuwa kikikutana na wadau mbalimbali wa usafirishaji na
kuwaeleza changamoto zinazowakabili abiria katika sekta ya usafirishaji
wa nchi kavu na majini hapa Nchini, ukiwemo urasimu unaofanyika katika
ununuzi wa tiketi ambapo kwa sasa wanalazimika kununua tiketi moja kwa
moja kwa mawakala na wapiga debe, ambapo wengi wao wamekuwa wakiwatapeli
abiria.
Hivyo
basi, kwa kuanzishwa mfumo wa kielektroniki utaondoa adha hiyo kwa
abiria na Serikali kukusanya mapato kwa uhakika na kuiwezesha Serikali
kutoa huduma bora kwa jamii na maendeleo kwa ujumla
0 comments:
Post a Comment