Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
DC
Hapi ameagiza wananchi wa eneo hilo kuendelea kukaa maeneo hayo baada
ya leseni ya uchimbaji kokoto eneo hilo kufutwa kutokana na uharibifu wa
miundombinu.
"Hatuwezi
kuhatarisha maisha ya wananchi 3000, tutawapeleka wapi, kwani wao siyo
wanakinondoni, kwani wao siyo watanzania" Alisema DC Hapi.
DC
Hapi ametoa maagizo kwa watendaji kuhakikisha kuwa wananchi hao
wanamilikishwa maeneo hayo kwao kufuata taratibu na sheria ambapo
itabidi maeneo hayo yapimwe na wananchi hao wawe wavumilivu maana kuna
baadhi ya maeneo yatatengwa kwa huduma za kijamii, ikiwemo vituo vya
Afya, Polisi na barabara.
Hata
hivyo DC Hapi amewatoa hofu wananchi wa maeneo hayo kuhusu kulipia
gharama za upimaji wa ardhi ambazo itabidi wachangie, huku akieleza kuwa
wataiandikia barua mamlaka ya chuo cha Ardhi ili waweze kutoa baadhi ya
wanafunzi ambao watafanya upimaji katika eneo hilo bure na kuwaondolea
wananchi gharama za ziada.
Kwa
upande wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Benjamini Sitta
amesisitiza kuwa serikali itakuwa bega kwa bega na wananchi wanyonge
kuhakikisha haki yao haipotei, huku Diwani wa Kata hiyo akihimiza
ushirikiano katika shughuli za maendeleo kwani maendeleo hayana chama,
hvyo ni vyema kuondoa itikadi.
Mkuu
wa Wilaya ya Kindoni Mhe Ally Hapi leo ametangaza msimamo wa serikali
ya wilaya ya Kinondoni kuwa wananchi wa Kunduchi Mecco na mji mpya Kata
ya Kunduchi waliokuwa na hofu ya kuondolewa kuwa hawataondolewa na
kwamba badala yake makazi yao yatapimiwa viwanja na watamilikishwa
rasmi.
Uamuzi huo umekuja baada ya mvutano wa miaka mingi baina ya manispaa ya Kinondoni na wananchi hao waliovamia eneo hilo ambalo awali lilitengwa kwa ajili ya machimbo ya kokoto. Katika mvutano huo ulioibua kesi mbili zilizoendeshwa kwa muda mrefu na hatimaye manispaa kushinda kesi hizo, uamuzi umefikiwa kuwa Manispaa ya Kinondoni haitawavunjia na kuwaondoa wananchi hao wapatao zaidi ya 3000 waliojenga eneo hilo.
Badala yake eneo hilo litapimwa ili kupanga vema mji na
kuruhusu maeneo ya huduma za msingi za jamii kama barabara, shule, afya
na zahanati kutengewa maeneo.
0 comments:
Post a Comment