Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » KAMPUNI NNE ZASHINDA KULETA MAFUTA NCHINI

KAMPUNI NNE ZASHINDA KULETA MAFUTA NCHINI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Imeandikwa na Mwandishi Wetu
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa PBPA, Modestus Lumato
KAMPUNI nne za mafuta zimeshinda zabuni za uletaji wa mafuta nchini kwa mwezi Septemba mwaka huu. Ufunguaji na utangazaji wa washindi wa zabuni ulifanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA), chini ya uenyekiti wa Ali Ahmed Saeed.
Kampuni zilizoshinda zabuni hiyo ni Trafigura Pte Limited, Addax Energy SA, Sahara Energy Resources Limited na GBP Tanzania Limited. Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa PBPA, Modestus Lumato, alifafanua kwamba zabuni hizo zinahusu uletaji wa jumla ya tani 360,000 za dizeli na tani 110,000 za petrol, mafuta ya taa na ndege.
Lumato alisema mahitaji ya mafuta yameongezeka, hivyo zabuni hizo zimehusisha uletaji mafuta ya nyongeza kwa mwezi Agosti kuziba upungufu uliojitokeza. “Kwa mwezi wa tisa tunategemea kuwa na meli saba, mahitaji ya mafuta yameongezeka sana…tutakuwa na meli saba yaani meli tatu kwa ajili ya dizeli tani 360,000 halafu meli tatu za petroli, meli ya mafuta ya ndege na mafuta ya taa,” alisema.
Lumato alitaja baadhi ya sababu za mahitaji ya mafuta kuongezeka ni pamoja na usafirishaji wa mazao mashambani kuongezeka kipindi cha mavuno na kuondolewa kwa kodi ya leseni ya usafirishaji.
Katika zabuni hiyo iliyoshuhudia kampuni ya Kitanzania ikishinda tenda ambayo ni GBP Tanzania Limited, Lumato alisema kwamba kwa siku nchi hutumia lita milioni 4.7 za dizeli, lita milioni 3.7 za petroli, lita 450,000 za mafuta ya ndege na lita 150,000 za mafuta ya taa.
CHANZO HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa