Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » MAONESHO YA SABASABA 2017: WATU ZAIDI YA 500 WATEMBEELA BANDA LA PSPF, ASILIMIA 70 YA HAO WAJIUNGA NA PSS

MAONESHO YA SABASABA 2017: WATU ZAIDI YA 500 WATEMBEELA BANDA LA PSPF, ASILIMIA 70 YA HAO WAJIUNGA NA PSS

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mwanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, akipitia taarifa ya michango yake, baada ya kukabidhiwa na Maafisa wa Mfuko huo, alipotembelea banda la PSPF kwenye maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam, leo Julai 12, 2017. Wakati wa maonesho hayo yakitarajiwa kufikia kilele kesho Alhamisi Julai 13, 2017, zaidi ya watu 500 wametembeela banda la Mfuko huo hadi mchana huu na kati ya hao asilimia 70 walifika kujiunga na Mpango wa uchangiaji wa Hiari, (PSS), unaomuwezesha mwananchi yeyote ambaye anafanya kazi za kumuingizia kipato kuwa mwanachama. Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko huo, Bw. Abdul Njaidi, alisema na kuongeza faida za mwanachama kujiunga na PSS, ni pamoja na kupata bima ya afya. (NA K-VIS BLOG/Khalfan Said)
 Afisa Msaidizi wa Uendeshaji wa PSPF, Bw.Mussa Mfaki, (kulia), akimkabidhi kadi ya kujiunga na PSPF kupitia Mpango wa uchangiaji wa Hiari, PSS, Bi.Damare B. Nampwani, leo Julai 12, 2017.
 Bi.Damare B. Nampwani, akionyesha kadi yake baada ya kukabidhiwa.
 Mwananchi akijaza fomu ya lujiunga na PSPF kupitia Mpango wa PSS, huku Mwanasheria kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti MHifadhi ya Jamii, (SSRA), Bi.Imani Masebu, (kulia), na Mhandisi Ally Shanjirwa, (katikati), wakishuhudia.
 Mwananchi akionyesha dole gumba baada ya kujaza fomu.

 Mwananchi akijaza fomu.
 Afisa Michango wa PSPF, Bw. Noah Amri, akiwa kwenye mashine ya kutoa vitambulisho vya papo kwa hapo.
 Afisa Uhusiano wa PSPF, Bi. Coleta Mnyamani, (kulia), akimkabidhi kadi ya uanachama ya PSPF, Afisa wa Polisi wa Usalama Barabarani, David S.Mlilo.
 Afisa Uhusiano wa PSPF, Bi. Coleta Mnyamani, (kulia), akimkabidhi kadi ya uanachama ya PSPF, Afisa wa Polisi wa Usalama Barabarani, Salvatory A. Chacky.
 Moja ya faida azipatazo Mwanachama wa PSPF,ni kuwa na uwezo wa kukopa kiwanja cha ujenzi wa nyumba na hapa ni Afisa Mipango Miji kutoka kampuni mshirika ya Adhi Plan Limited, Bi. Anna Lukando, (kulia), akimpatia maeelzo ya jinsi gani mwanachama anaweza kupata mkopo wa kiwanja au kununua kabisa.
Hiki ndio kikosi kazi cha PSPF ambacho kwa takriban wiki moja na nusu kimekuwa kikitoa huduma kamambe kwenye banda la Mfuko huo kwenye jengo la Wizara ya Fedha na Mipango kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, ambako kumekuwa na maonesho ya 41 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam. Kutoka kushoto waliosimama ni Isack Kimaro, Mussa Mfaki, Chaula Miteko, Mhandisi Ally Shanjirwa, Abdul Njaidi, Noah Amri,Win-God, Bw.Msina. Waliokaa kutoka kushoto, ni Bi. Coleta Mnyamani, Bi. Mariam Saleh, Bi. Irine Musetti na Bi. Asmahan H.Haji.
Win-God, (kushoto), Afisa wa uendeshaji msaidizi wa PSPF, akiwahudumia wananchi waliofika banda la Mfuko huo leo Julai 12, 2017.
 Afisa Uendehsji wa PSPF, Bw. Isack Kimaro, (kulia), akiagana na Mwananchi huyu aliyefika kupatiwa huduma
Afisa Uendeshaji wa PSPF, anayeshughulikia Mpango wa Uchangiaji wa Hiari, (PSS), Bi. Asmahan Haji (kulia), akimsaidia mwanachama huyu wa PSPF kuelewa michango yake.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa