Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na. Bushiri Matenda-MAELEZO
Serikali
imesisisitiza kuwa matumizi ya mitandao lazima yazingatie sheria
zilizopo na kuheshimu maadili, utamaduni na ustaarabu wa watumiaji.
Hayo
yameelezwa jana na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo,
Anastazia Wambura alipokuwa akifunga mkutano juu ya njia mpya za
mawasiliano ulioandaliwa na Serikali ya Tanzania na China uliofanyika
Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere Jijini Dar es
Salaama.
“Matumizi ya mitandao ni lazima yasimamiwe, yaratibiwe
na yafanyike kwa mujibu wa sheria ili mitandao iweze kuendelea na
kuimarika chini ya utawala wa sheria,” amesema Wambura.
Aliongeza
kuwa katika hali ya sasa ya matumizi ya mitandao ni lazima juhudi zaidi
ziongezwe katika kuimarisha maadili na kuhimiza ustaarabu na msisitizo
zaidi uwekwe katika ufundishaji wa maadili katika matumizi ya intaneti
ili kusaidia kukua zaidi kwa mitandao katika hali salama na yenye
maadili.
Wambura aliwaambia washiriki wa mkutano huo kuwa,
Serikali ya Tanzania inayapa uzito mkubwa maendeleo ya intaneti, kwa
kuwa intaneti ni moja ya njia muhimu katika kusaidia kuinua hali za
maisha ya wananchi wake kupitia matumizi ya teknolojia ya habari na
mawasiliano.
“Tangu mwaka 1995 ambapo Tanzania iliunganishwa na
huduma za intaneti, tumekuwa tukichukua hatua kuhakikisha matumizi
sahihi ya huduma hiyo ambapo tumetunga sheria na mfumo wa usimamizi na
usalama wake, pia tunaendelea kuimarisha miundombinu ya teknolojia ya
habari na mawasilino pamoja na kufanya maisha ya wananchi wetu kuwa
mazuri zaidi kupitia matumizi ya teknolojia hiyo” alibainisha Wambura.
Aidha
Wambura alieleza kuwa kila siku Dunia inashuhudia kasi kubwa ya
maendeleo ya teknolojia ya habari kupitia intaneti ambayo yameifanya
Dunia kuwa kijiji na kurahisisha mawasiliano ambapo watu wanawasiliana
kwa urahisi wakati wote bila vizuizi.
Alisema kuwa upo umuhimu
kwa Serikali hizo mbili kuweka mazingira wezeshi kisheria na uratibu
utakaoweza kuhamasisha ukuaji wa matumizi ya teknolojia ya habari na
mawasiliano na kuvutia ubunifu kwa kizazi cha sasa.
“Ushirikiano
unaozingatia haki, usawa na kuaminiana ni kitu kisichoepukika ikiwa
Dunia inataka kuwa na mtandao salama na wenye manufaa kwa wote,”
alifafanua Wambura.
Mkutano huo umehudhuriwa na wadau wa habari
kutoka Tanzania na China ambapo uliongozwa na kauli mbiu ya “Maendeleo
ya vyombo vya habari yanayochochewa na ubunifu.
0 comments:
Post a Comment