Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Thobias Robert – MAELEZO.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli
amepongezwa na Shirika lisilo la kiserikali la ‘We are all needed’ (WAN)
kwa agizo lake la kukataza wanafunzi wenye ujauzito kuendelea na masomo
katika shule za Serikali.
Pongezi
hizo zimetolewa leo Jijijni Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Shirika
hilo, Bi Salome Lwena alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari
kuhusu kuunga mkono agizo hilo.
Bi.
Lwena amesema kuwa shirika lake liko tayari kumuunga mkono Rais
Magufuli katika harakati za kukuza na kuendeleza maadili nchini ikiwemo
suala la kupunguza mimba za utotoni.
“Sisi
WAN tunaunga mkono kauli ya Mh. Rais kuhusu suala la ukatazaji mimba
kwa shule za Serikali za Msingi na Sekondari ili wanafunzi hao
wasiathiri wanafunzi wengine kwani wanafunzi wakipata ujauzito
wanaathirika kisaikolojia,”alifafanua Mwenyikiti huyo.
Bi.
Lwena aliongeza kuwa kauli ya Rais Magufuli imewapa nguvu ya kuzidi
kutoa elimu ya kuzuia mimba za utotoni kwa wanafunzi ili wasome hadi
watakapokamilisha ndoto zao kwani linajihusisha na shughuli ya kutoa
elimu ya kujitambua kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari hapa
nchini.
Bi.
Lwena alieleza kuwa, kwa sasa Shirika hilo lina mradi utakaofanyika
nchi nzima ujulikanao kama “Protect your dream” utakaotolewa katika
shule za Msingi na Sekondari nchini kwa kushirikiana na wataalam wa afya
kutoka Wizara ya afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na
mashirika ya binafsi ili kuokoa vijana na kulinda maadili ya Mtanzania.
Kwa
upande wake Katibu wa shirika hilo, Romanus Dominicus alitoa wito kwa
wazazi na walezi kuendeleza maadili katika Taifa kwani hakuna Taifa
lililoendelea Duniani kwa kuharibu maadili na nidhamu ya watoto.
“Umefika
wakati kwa mashirika mengine, wazazi, walezi na walimu kushirikiana
kutoa elimu sahihi na salama kwa watoto wetu wa kike na wa kiume kuhusu
madhara ya vitendo vya ngono na mimba za utotoni,” alisema Dominicus.
Dominicus aliongeza kuwa Shirika
la WAN pamoja na wote wenye mapenzi ya dhati na watoto wa Tanzania
wanahitaji kuwa na kizazi bora kitakachorithi na kumudu kuiendeleza
Tanzania kwani kurithi nchi ni jambo jingine na kumudu kuiendeleza ni
jambo jingine.
Agizo
la kutoendelea na masomo kwa mtoto wa kike aliyepata ujauzito kwa shule
za Msingi na Sekondari lilitolewa na Rais Magufuli mwezi June mwaka huu
alipokuwa ziarani mkoani Pwani.
0 comments:
Post a Comment