Na Thobias Robert.
Sekta
ya utalii nchini imeendelea kukuza na kuongeza mapato ya serikali kwa
kuchangia zaidi ya asilimia 17 ya pato la taifa, huku ikitazamiwa
kuongezeka katika mwaka huu wa fedha.
Hayo yalisemwa Jana na
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za taifa (TANAPA) Bwana Allan
Kijazi wakati akizungumza katika kipindi cha TUNATEKELEZA” kinachorushwa
na Televisheni ya Taifa (TBC1).
“Utalii unatoa mchango mkubwa
sana katika uchumi wa nchi hii, kwa sasa hivi unakisiwa kwamba
unachangia kama asilimia 17.2 ya pato la taifa na asilimia 25 ya fedha
ya kigeni,” alisema Bw. Kijazi. huku akisisitiza kuwa TANAPA watazidi
kulinda na kuendeleza hifadhi zilizopo nchini ili zizidi kuongeza pato
la taifa kwa maendeleo ya watanzania wote.
Mkurugenzi huyo wa
TANAPA alisema kuwa katika mwaka wa fedha 2016/2017 TANAPA ilichangia
kiasi cha billion 27 kwenda Mfuko wa Taifa wa serikali na matarajio yao
katika kuchangia mfuko wa fedha wa Taifa kwa mwaka huu wa fedha
2017/2018 ni bilioni 33.4 hii ni kwa sababu ya kuongezeka kwa Watalii
kutoka nje ya nchi.
Aliongeza kuwa Tanzania ina vivutio vingi
kama vile Mito, Mabonde, Milima, lakini hifadhi za Taifa kama Vile
Ngorongoro, Serengeti, Gombe, Ruaha ndizo zinazoongoza kwa kuchangia
pato la taifa kwa zaidi ya asilimia 80 ikilinganishwa na vivutio
vingine.
Bwana Kijazi aliongeza kwa kusema kuwa, utalii nchini
umekuwa ukikuunaongezeka kila mwaka ambapo kwa takimwu walizo nazo
zinaonesha kuwa, ongezeko la watalii kwa miaka mitano iliyopita limekuwa
lilkiongezeka kwa asilimia 4 hadi 7 kila mwaka.
Kuongeza kwa
watalii hasa katika hifadhi za Taifa kunatokana na TANAPA kujitangaza
zaidi katika nchi mbalimbali duniani kupitia Mitandao ya kijamii,
Makampuni binafsi ndani na nje ya nchi, Balozi za Tanzania katika
mataifa ya Nje, Vilabu mbalimbali vya Ulaya na Amerika pamoja Vyombo vya
Habari vya kimataifa kama vile CNN na BBC.
Mkurugenzi Kijazi
alisema kuwa, Mataifa yanayoongoza kutembelea hifadhi za taifa ni pamoja
na Marekani, Ujerumani, Uingereza, Italia, Ufaransa, pamoja na Hispania
huku akitaja kuwa vivutio vya utalii vilivyopo Nchini hasa hifadhi ni
vya kipekee, mazingira mazuri, hali ya hewa pamoja na amani na utulivu
uliopo nchini ndiyo sababu zinazowavutia watalii kuongezeka kila
mwaka.
Pamoja na kukua na kuongezeka kwa utalii nchini
kunakopelekea kuongeza la Taifa, Mkurugenzi Kijazi alisema kuwa, utalii
wa ndani bado ni changamoto kwani watalii wengi wanatoka nje ya Nchi
huku wazawa wakishindwa kuzuru maeneo mbalimbali ya utalii ili
kujionea fahari ya nchi yao hivyo ametoa wito kwa Watanzania kutembelea vivutio hivyo ili kukuza na kuongeza pato la Taifa.
Hivi
karibuni Mtandao wa SafariBookings.com unaojihusisha na masuala ya
ukuzaji wa safari za kitalii barani Afrika uliitaja Tanzania kama
kivutio kizuri cha safari za watalii barani humu.
0 comments:
Post a Comment