Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » WAKAZI WA DAR, PWANI KUKOSAMA MAJI KWA SAA KADHAA KUPISHA UBORESHAJI WA MTAMBO MPYA WA UZALISHAJI MAJI WA RUVU JUU

WAKAZI WA DAR, PWANI KUKOSAMA MAJI KWA SAA KADHAA KUPISHA UBORESHAJI WA MTAMBO MPYA WA UZALISHAJI MAJI WA RUVU JUU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.


Shirika la MajiSafi na Majitaka Dar-es-salaam (DAWASCO), linawatangazia wateja wake wote wa jiji la Dar-es-salaam, pamoja na Mji wa Kibaha Mkoani Pwani kuwa mtambo wa uzalishaji Maji wa Ruvu Juu utazimwa kwa wastani wa Saa 8, kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 11:00 jioni, siku ya Jumatatu tarehe 31/07/2017.

Sababu ya kuzimwa kwa Mtambo : Kumruhusu Mkandarasi (WABAG), kukamilisha Mfumo wa umeme katika mtambo mpya wa uzalishaji Maji wa Ruvu Juu uliopo Mlandizi mkoani Pwani.

Maeneo yatakayoathirika na Kuzimwa Kwa Mtambo huu:

Mlandizi Mjini, Ruvu Darajani, Vikuruti, Disunyara, Kilangalanga, Janga, Mbagala, Visiga, Maili 35, Zogowale, Misugusugu, Tanita, Kibondeni, Kwa Mathias, Nyumbu, Msangani, Kwa Mbonde, Picha Ya Ndege, Sofu, Lulanzi, Gogoni, Kibamba, Kibamba Njia Panda Shule Kibwegere, Mloganzira, Kwembe, Kibamba Hospitali, Kwa Mkinga, Luguruni, Kimara, Ubungo, na baadhi ya maeneo ya Tabata.

Toa taarifa Dawasco kupitia vituo vya wateja  Dawasco kimara 0743-451865, Dawasco Tabata 0743-451867, Dawasco Kibaha 0743-451875.

Dawasco inawaomba wateja kutunza Maji ya kutosha pindi Mtambo utakapokamilika
Kwa taarifa zaidi wasiliana nasi: Kituo cha huduma Kwa wateja 0800110064 (BURE) au Tembelea: www.dawasco.go.tz

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa