Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Naibu
Kamishna wa Polisi (DCP), Hussen Laisser akizungumza na waandishi wa
habari mara baada ya kufunga mafunzo ya siku tano yaliyohusu udhibiti
wa mionzi yaliyofanyika kwenye hoteli ya New Afrika jijini Dar es salaam
na kuhudhuria na maofisa wa Interpool kutoka nchi za Afrika Mashariki,
Kati na na Kusini mwa Afrika.
Na Neema Mathias na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.
Wadau
wa masuala ya mionzi wameaswa kufanyia kazi maarifa na ujuzi waliopata
katika semina ya siku 5 ya namna ya kufahamu na kudhibiti vyanzo vya
mionzi.
Wito
huo umetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Naibu Kamishna wa Polisi
(DCP), Hussen Laisser alipokuwa akifunga mafunzo hayo ambayo kwa mara ya
kwanza yamefanyika nchini.
DCP
Laisser amesema kuwa mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na Wizara ya Nishati
ya Marekani na Sekretari ya Interpol ya nchini Ufaransa yalihusisha
jumla ya wadau wa masuala ya mionzi 59 kutoka katika nchi tisa zikiwemo
za Botswana, Afrika Kusini, Malawi, Ethiopia, Kenya, Mauritius, Tanzania
pamoja na Zambia.
“Vyeti
mlivyotunukiwa leo vimewatambua kama wawakilishi wa wengi waliobaki
katika nchi zenu hivyo mnaporudi katika nchi zenu msitumie vyeti hivyo
kama mapambo bali mtumie ujuzi mlioupata kuwaelimisha na wengine,”
alisema DCP Laisser.
DCP
Laisser ameongeza kuwa mionzi ina manufaa kwa jamii lakini isipotumika
au kutunzwa vizuri inaleta madhara hivyo mafunzo hayo yamelenga
kuwaandaa wadau mbalimbali wa masuala hayo kufahamu namna ya kugundua,
kuchunguza na kudhibiti mionzi.
Aidha,
DCP Laisser amewatoa hofu Watanzania kuwa hakuna uhalifu unaotokana na
mionzi lakini lengo la mafunzo hayo ni kujiandaa kupambana na matukio ya
kiuhalifu ambayo yanaweza kutokea.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Teknolojia ya Mionzi, Dkt. Firmi Banzi
amesema kuwa sababu kubwa ya kukosekana kwa mafunzo ya masuala ya mionzi
kwa Tanzania ni ukosefu wa wataalam na vifaa kwani vifaa hivyo vina
gharama kubwa.
“Kwa
kuwa mionzi haiwezi kugundulika kwa kutazamwa, kunuswa au kuguswa bali
huitaji vifaa maalum hivyo tunawashukuru wafadhili wa mafunzo haya kwa
sababu baada ya mafunzo wanatukabidhi vifaa vitakavyotumika kutambua
mionzi,” alisema Dkt. Banzi.
Mafunzo hayo yamefanyika mara sita katika nchi tofauti tofauti, kwa Tanzania ni mara ya kwanza mafunzo hayo kufanyika.
0 comments:
Post a Comment