Na. Paschal Dotto na Georgina Misama –MAELEZO
Chama
Cha Wapangaji Tanzania (TTA) kimeiomba Serikali kupitia Wizara ya Ardhi
Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuunda Mamlaka Maalumu ya kudhibiti
biashara ya kupangisha nyumba za makazi (Tenancy Regulatory Board).
Akizungumza
na Waandishi wa Habari leo Jijini Dar es salaam, Katibu Mkuu wa TTA Bw.
Ndumey Mukama alisema kwamba biashara ya kupangisha nyumba kwa ajili ya
makazi imekuwa huria kiasi cha kila mmiliki wa nyumba kujipangia bei
kulingana na matakwa yake.
“Kukiwa
na Mamlaka maalum ya kushughulikia biashara ya upangishaji nyumba za
makazi, kutaweka misingi ya haki na usawa kwa Watanzania katika matumizi
ya nyumba kwa wapangaji”, alisema Mukama.
Akiongelea
maslahi ya Taifa, Mwanasheria wa Chama cha Wapangaji Tanzania Bi.
Pamela Kihumo alisema kwamba kuundwa kwa Mamlaka ya kudhibiti biashara
ya wapangaji wa nyumba za makazi kutachochea kuongeza mapato kutokana na
wamiliki wa nyumba hizo kulipa kodi kama wafanya biashara wengine.
Aidha,
Pamela alisema kwamba, uwepo wa Mamlaka utaondoa malalamiko mengi ya
utapeli kutoka kwa madalali ambao hujiweka katikati ya wapangaji na
wamiliki wa nyumba kwa nia ya kujipatia pesa kwa kazi ya kumuunganisha
mpangaji na mpangishaji.
Aliongeza
kuwa Chama hicho kipo kuhakikisha kuwa raia wa Tanzania wa bila kujali
umri, rangi na jinsia zote ambao ni wapangaji wa nyumba za makazi,
biashara au mashamba wanalindwa wakiwa ni wateja wa huduma ya upangaji.
Alieleza
kuwa TTA inapendekeza kuwa ni muhimu kuwa na Sera ya Nyumba (Housing
policy), Sheria zaUupangaji (Tenancy Legislation) chini ya Mamlaka ya
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo na Makazi ili kuweka mazingira safi
kwa wapangaji.
Chama
cha wapangaji Tanzania kilianzishwa mwaka 1985 kikiwa na dhamira ya
kuweka mwongozo na mwelekeo wa kusaidia wananchi kupata makazi bora kwa
wapangaji wote ndani ya Tanzania na kutoa huduma iliyobora katika
mahusiano ya pande mbili yaani mpangaji na mpangishaji
Chama
kina mahusiano mazuri na Serikali ya Jamhuri Muungano wa Tanzania
kupitia Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) pamoja na Wizara ya Ardhi,
Nyumba na Maendeleo na Makazi na wanafanya kazi kwa pamoja katika
kutambua uhitaji wa makazi kwa watanzania.
Aidha,
TTA inatambulika kimataifa na kuiwakilisha Tanzania katika mahusiano ya
karibu na vyama vingine Duniani kama Shirika la Makazi duniani
(UN-Habitat) tawi la Tanzania, Vyama vya Wapangaji vya Afrika pamoja na
Chama Kikuu cha Wapangaji Duniani (International Union of Tenants).
0 comments:
Post a Comment