Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » WASICHANA WAISHUKURU TGGA KUFANIKISHA ZIARA YA MAFUNZO NJE YA NCHI

WASICHANA WAISHUKURU TGGA KUFANIKISHA ZIARA YA MAFUNZO NJE YA NCHI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Wasichana wanachama wa Tanzania Girl Guides wakiwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, wakitokea kwenye ziara ya programu ya miezi sita ya mafunzo ya kubadilisha uzoefu katika masuala ya utamaduni, uongozi na maadili. Kutoka kushoto ni Ummy Mwabondo alikwenda Zambia, Edna Chembele (Zimbabwe), Elizabeth Betha (Madagascar) na Farida Mjoge aliyekuwa Uganda. PICHA, HABARI NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG

WASICHANA wanne wanachama wa Chama cha Tanzania Girl Guides (TGGA) wamerejea nchini kutoka kwenye programu ya mafunzo ya miezi sita katika nchi mbalimbali za Afrika.

Wasichana hao waliokuwa kwenye mafunzo ya kubadilishana uzoefu katika mambo ya utamaduni, uongozi na maadili katika nchi za Zambia, Zimbabwe, Madagascar na Uganda wameipongeza TGGA kwa kufanikisha ziara hiyo yenye mafanikio makubwa katika maisha yao.

Walipowasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam jana kwa ndege ya Kenya Airways, walilakiwa na Katibu Mkuu wa TGGA, Grace Shaba, ndugu jamaa na marafiki huku wengine wakivishwa mashada na kupatiwa zawadi mbalimbali. Wasichana waliokwenda kwenye mafunzo hayo ni; Ummy Mwabondo, Elizabeth Betha, Edna Chembele na Farida Mjoge ambao kila mmoja anaeleza jinsi alivyonufaika na ziara hiyo.

Elizabeth Betha ambaye programu yake aliifanyia Madagascar, anaeleza kuwa Wananchi wa Kisiwa hicho utamaduni wao ni tofauti kabisa na wa Tanzania na  maeneo mengine ya Afrika, ambapo mara nyingi hutumia lugha yao ya asili na  kifaransa kama Lugha yao ya Taifa, ni wakarimu sana na wana upendo.

Anasema kuwa licha ya kuwafundisha mambo mengi ya Tanzania ikiwemo utamaduni, mapishi ya vyakula mbalimbali, lugha ya kiswahili na vivutio mbalimbali vya kitalii pia wakiwa huko walipanda  miti, kufundishana kwa uwazi masuala ya hedhi salama, kuzuia ukatili wa kijinsia pamoja na kuwapa stamina ya kujiamini na kujithamini.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa