Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mkuu wa Majeshi wa India, Admiral
Sunil Lanba Ofisini kwake jijini Dar es salaam Julai 28, 2017. Kulia ni
Mkuu wa Majeshi, Jeneral Venance Mabeyo. (Picha na Ofisi ya Waziri
Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mkuu wa Majeshi wa India , Admiral
Sunil Lanba (kulia kwake) pamoja na ujumbe wake, Ofisini kwake jijini
Dar es salaam Julai 28, 2017. Kushoto kwake ni Mkuu wa Majeshi, Jeneral
Venace Mabeyo.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Majeshi
wa India Admiral Sunil Lanba (wapili Kushoto) na Mkuu wa Majeshi
nchini, Jeneral Venance Mabeyo (kushoto) baada ya mazungumzo yao,
Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Julai 28, 2017. Kushoto ni
Balozi wa India Nchini, Sandeep Arya.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Majeshi
wa India Admiral Sunil Lanba (kulia kwake ) na Mkuu wa Majeshi nchini,
Jeneral Venance mabeyo (kushoto kwake ) baada ya mazungumzo yao,
Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Julai 28, 2017. Kushoto ni
Balozi wa India Nchini, Sandeep Arya.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akijadili jambo na Mkuu wa Majeshi wa India,
Admiral Sunil Lanba (kulia) baada ya mazungumzo yao Ofisini kwa Waziri
Mkuu jijini Dar es salaam Julai 28, 2017 . Wapili kulia ni Mkuu wa
Majeshi Nchini, Jeneral Venance Mabeyo na kushoto ni Balozi wa India
Nchini, Sandeep Arya.v
WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Tanzania itaendeleza
ushirikiano na Serikali ya India katika nyanja mbalimbali ikiwemo ya
ulinzi.
Ametoa
kauli leo (Ijumaa, Julai 28 , 2017) alipokutana na kufanya mazungumzo
na Mkuu wa Majeshi wa India, Bw. Admiral Sunil Lanba jijini Dar es
Salaam.
Waziri
Mkuu amesema Tanzania na India ni nchini ambazo zina uhusiano mzuri na
wa muda mrefu, ambapo ameahidi kwamba Serikali itaendelea kuudumisha.
“Ushirikiano
wa Tanzania na India ni wa kihistoria, hivyo tutauendeleza na
kuudumisha. India tunashrikiana nao katika sekta za uchumi, afya, elimu
na ulinzi.”
Waziri
Mkuu ameishukuru Serikali ya India kwa ufadhili walioutoa kwa Tanzania
katika kuimarisha miradi ya maji kwenye mikoa mbalimbali nchini.
Pia
Waziri Mkuu amewakaribisha raia wa India kuja kutembelea maeneo ya
utalii nchini ukiwemo mlima wa Kilimanjaro, mbuga za wanyama na visiwa
vya Zanzibar.
Kwa
upande wake, Mkuu wa Majeshi wa India, Bw. Lanba ameishukuru Serikali
ya Tanzania kwa ushirikiano inaoutoa kwa Serikali ya India hususan
katika masuala ya ulinzi.
Amesema
wamefanya kikao na Mkuu wa Majeshi nchini Generali Venance Mabeyo
ambapo katika mazungumzo yao wameweka mikakati ya kushirikiana katika
kuimarisha ulinzi hususan maeneo ya mipakani pamoja na masuala ya
mafunzo.
0 comments:
Post a Comment