Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mwanafunzi bora nafasi ya tatu kitaifa katika masomo ya biashara wa shule ya Tusiime, Rashid Abdalah aliyevaa flana, akifurahia na kupongezwa na wanafunzi wa kidato cha tano wa shule hiyo alipokwenda kuwatembelea na kuwadokeza siri ya mafanikio yake.
MWANAFUNZI
wa shule ya Sekondari ya Tusiime, Rashid Abdalah, aliyeshika nafasi ya
tatu kitaifa kwa masomo ya biashara amesema nia yake ni kusoma hadi
ngazi ya Shahada ya Uzamivu (PhD).
Akizungumza
leo shuleni hapo Rashid amesema ndoto yake ya miaka mingi ni kuwa
mkaguzi wa hesabu hivyo amenuia kusoma kwa bidii hadi afikie ngazi hiyo.
“Naamini
nitafikia malengo yangu kwa kuwa najua siri ya kufika huko ni juhudi,
kujitambua na kuwasikiliza walimu, hakuna kingine zaidi ya
kuwa makini na masomo na kuwa makini,” alisema Rashid ambaye alianzia
kidato cha pili shuleni hapo mwaka 2012.
Amesema
juhudi za walimu katika kufuatilia maendeleo ya wanafunzi na mazingira
mazuri ya shule, ushirikiano mzuri na wanafunzi wenzake ni baadhi ya
mambo ambayo yamekuwa chachu ya mafanikio yake.
Aidha
amewaasa wanafunzi waliobaki shuleni hapo kujitambua wamefuata nini
shuleni na kufuatilia kila wanachofundishwa na walimu wao ili mwisho wa
siku wapate mafanikio kama yake.
“Kufaulu
haiwezi kuwa muujiza ni juhudi tu na kusikiliza mafundisho na maelekezo
ya walimu, lazima mtambue kuwa walimu wanataka mfaulu hivyo
mkiwasikiliza na kuwafuata mtafaulu kwa viwango vya juu sana,” amesema
Rashid alipokuwa akizungumza na wanafunzi wa kidato cha tano shuleni
hapo.
Mkuu
wa shule hiyo, Emil Rugambwa, amesema mafanikio ya shule hiyo kwenye
matokeo ya kidato cha sita ni mwendelezo wa mafanikio kwenye matokeo ya
kitaifa ambayo shule imekuwa ikiyapata kuanzia yale ya darasa la nne,
darasa la saba, kidato cha pili na cha nne.
0 comments:
Post a Comment