Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akionyesha Jarida la Mpango Mkakati la Shirikisho la Masumbwi Tanzania (BFT) mara baada ya kufanya nao mazungumzo katika Ofisi za Wizara 01 Agosti, 2017 Jijini Dar es Salaam.
Na Benedict Liwenga-WHUSM.
Waziri
wa Habari Utamaduni Sanaana Michezo, Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
amewaahidi Shirikisho la Masumbwi Tanzania (BFT) kuwatatulia kero ya
eneo la kufanyia mafunzo pamoja na ofisi ambalo limekuwa likiwakabili
kwa muda mrefu zikiwemo na changamoto nyingine za Shirikisho hilo.
Mhe.
Mwakyembe ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam wakati alipokutana na
kufanya mazungumzo na baadhi ya Viongozi na wajumbe mbalimbali wa
shirikisho hilo ikiwa ni sehemu ya kutambua utendaji kazi wao na
changamoto zinazowakabili ili ziweze kutatuliwa.
Dkt.
Mwakyembe amesema kwamba, kutokana na tatizo la ukosefu wa eneo rasmi
la ofisi na sehemu ya kufanyia mafunzo, yeye atawasiliana na Waziri wa
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi ili kuona
namna gani wanaweza kupata eneo kwa ajili ya kulisaidia shirikisho hilo
kwa ajili ya kujenga ofisi na eneo la kufanyia mazoezi.
Sambamba
na hilo, ameupongeza uongozi wa shirikisho hilo kwa kazi wanazozifanya
na kuwataka wazidi kushirikiana na Baraza la Michezo la Taifa (BMT)
hususani katika kupeana taarifa zinazohusu maendeleo ya mchezo wa
masumbwi nchini.
“BFT
jitahidini muwe na ushirikiano wa karibu na Baraza la Michezo la Taifa
(BMT) na msifanye mambo yenu kimya kimya, muwasiliane kwa karibu na BMT
kwani hii itasaidia Wizara kushughulikia kero zenu mbalimbali kuliko
mkichelewa kutoa taarifa mapema”, alisema Dkt. Mwakyembe.
Aidha,
amewahakikishia kuwa, yupo tayari kutafuta wafadhili ndani na nje ya
nchi ili waweze kulisaidia shirikisho hilo kutatua kero za uhaba wa
vifaa, rasilimali fedha pamoja na ukosefu wa mafunzo kwa makocha.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo, Yusuph Singo amelitaka
shirikisho hilo kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu za Serikali ikiwemo
kujenga tabia ya ulipaji kodi, kuwaelimisha Wanamasumbwi kuachana na
tabia chafu wanapokuwa michezoni pamoja na kuachana na kujihusisha na
madawa ya kulevya.
Kwa
upande wao Viongozi wanaounda shirikisho hilo pamoja na wajumbe kwa
pamoja wamemuahidi Waziri Mwakyembe na Wizara kwa ujumla kuzingatia
masuala mbalimbali ikiwemo kuboresha suala la mawasiliano kati ya
Shirikisho na Wizara, kufuatilia suala la mikataba mbalimbali na
uwajibikaji yakinifu.
0 comments:
Post a Comment