Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mwenyekiti
wa Taasisi ya sekta binafsi nchini (TPSF) Dr. Reginald Mengi
akizungumza wakati akifungua mkutano wa Taasisi
za Sekta Binafsi za Tanzania na Kenya zilizokutana jijini Dar es salaam
kujadili kwa pamoja namna ya kuondoa vikwazo vya kufanya biashara baina
ya wafanyabiashara wa nchi hizo mbili uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Gavana wa Taasisi ya Sekta Binafsi ya Kenya – KEPSA Bw. George Owuor akimpongeza Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta binafsi
nchini (TPSF) Dr. Reginald Mengi kwa kutoa risala nzuri ya ufunguzi wa mkutano huo.
Gavana
wa Taasisi ya Sekta Binafsi ya Kenya – KEPSA Bw. George Owuor
akiwasilisha mada kuhusu kupunguza pengo la biashara
kati ya Tanzania na Kenya na kutumia fursa zilizopo na kutanua biashara
nje ya mipaka katika mkutano wa Taasisi za Sekta Binafsi za Tanzania na
Kenya zilizokutana jijini Dar es salaam kujadili kwa pamoja namna ya
kuondoa vikwazo vya kufanya biashara baina ya
wafanyabiashara wa nchi hizo mbili uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Meneja
anayeshughulikia Utafiti, Uchambuzi na Sera wa Taasisi ya Sekta Binafsi
ya Kenya – KEPSA, Victor Ogalo (kushoto)
akitoa mada kuhusu changamoto za kisera za Tanzania na Kenya katika
mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam. Kulia walioketi ni Gavana
wa Taasisi ya Sekta Binafsi ya Kenya – KEPSA Bw. George Owuor na
Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta binafsi nchini (TPSF)
Dr. Reginald Mengi wakifuatilia kwa umakini mada hiyo.
Mkurugenzi
Mtendaji wa TPSF Bw. Godfrey Simbeye (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa
kampuni ya Alaska Tanzania, Jennifer
Bash wakifuatilia mada mbalimbali zikizokuwa zikiwasilishwa ukumbini
hapo katika mkutano wa Taasisi za Sekta Binafsi za Tanzania na Kenya
zilizokutana jijini Dar es salaam kujadili kwa pamoja namna ya kuondoa
vikwazo vya kufanya biashara baina ya wafanyabiashara
wa nchi hizo mbili uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Pichani
juu na chini ujumbe wa Tanzania na Kenya ulioshiriki mkutano wa Taasisi
za Sekta Binafsi za Tanzania na Kenya
zilizokutana jijini Dar es salaam kujadili kwa pamoja namna ya kuondoa
vikwazo vya kufanya biashara baina ya wafanyabiashara wa nchi hizo mbili
uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Gavana wa Taasisi ya Sekta Binafsi ya Kenya – KEPSA Bw. George Owuor na mwenyeji wake Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta
binafsi nchini (TPSF) Dr. Reginald Mengi katika mkutano huo.
Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF Bw. Godfrey Simbeye akijibu maswali kwa waandishi wa habari (hawapo pichani). Kulia ni Mwenyekiti
wa Taasisi ya sekta binafsi nchini (TPSF) Dr. Reginald Mengi.
Akizungumza katika mkutano huo Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF Bw. Godfrey Simbeye amesema mkutano huo umeitishwa kutokana na kujitokeza vikwazo vya kufanya biashara baina ya Wafanyabiashara wa Tanzania na Kenya, jambo linalokwamisha malengo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya kujenga uchumi unaoongozwa na sekta Binafsi.
MWENYEKITI
wa Taasisi ya sekta binafsi nchini (TPSF) Dr. Reginald Mengi amezitaka
Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kushirikiana katika
kutumia utajiri wake mkubwa wa raslimali kunufaika kiuchumi.
Ushirikiano
huo ni pamoja na kuzindeleza raslimali hizo na kutumia nembo moja ya
kibiashara ili kuzalisha mabilionea wakubwa duniani.
Mwenyekiti
huyo alisema hayo katika mkutano wa Taasisi za Sekta Binafsi za
Tanzania na Kenya zilizokutana jijini Dar es salaam kujadili
kwa pamoja namna ya kuondoa vikwazo vya kufanya biashara baina ya
wafanyabiashara wa nchi hizo mbili.
Pamoja
na kutoa wito huo Dk Mengi pia amempongeza Rais wa Tanzania Dk John
Pombe Magufuli pamoja na serikali yake kwa kuwa mstari wa
mbele kuboresha ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na Kenya.
Aidha alisema dhamira yake ya kuigeuza Tanzania kuwa nchi ya viwanda itasaidia kuwakwamua Watanzania kutoka katika umaskini.
Katika
mazungumzo hayo ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Mwenyekiti wa Taasisi
ya Sekta Binafsi Tanzania –TPSF Dr Reginald Mengi na Ujumbe
wa Kenya umeongozwa na Gavana wa Taasisi ya Sekta Binafsi ya Kenya –
KEPSA Bw. George Owuor.
Akizungumza katika mkutano huo Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF Bw. Godfrey Simbeye amesema mkutano huo umeitishwa kutokana na kujitokeza vikwazo vya kufanya biashara baina ya Wafanyabiashara wa Tanzania na Kenya, jambo linalokwamisha malengo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya kujenga uchumi unaoongozwa na sekta Binafsi.
Kwa
upande wake Kiongozi wa Ujumbe wa KEPSA Bw. George Owuor amesema
Wafanyabiashara wa Kenya wanapenda sana kushirikiana kibiashara
na wenzao wa Tanzania, na wangependa kuona vikwazo vinavyokwamisha
mahusiano ya kibiashara vinaondolewa.
0 comments:
Post a Comment