Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mama
Gertrude Mongella(katikati) akiwasisitiza wanamke kuwa hakuna haja ya
mwanamke kulalamika, kuomba, kulia lia pamoja na kulaumu ili kuweza
kuwapata wanawake wachapa kazi kwenye mkutano uliowakutanisha wanawake
mashuuri hapa barani Afrika.
Mwenyekiti
wa Kigoda cha Mwalimu Nyerere, Profesa Penina Mlama akizungumza jambo
kwa wanawake waliofika kwenye kongamano hilo leo jijini Dar es Salaam
Prof.
Ruth Meena akiwasilisha mada kwa wanawake pamoja na viongozi na baadhi
ya wanawake mashujaa wa barani Afrika waliofika kwenye kongamano la uso
kwa uso lililofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Dk. Gennet Zewide
Baadhi
ya wanawake waliofika kwenye kongamano hilo wakichangia mada pamoja na
kuuliza maswali kwenye kongamano hilo lililofanyika leo jijini Dar es
Salaam.
Picha ya Pamoja
Mkurugenzi
Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Bi. Lilian Liundi
akizungumza kwenye mkutano wa ana kwa ana na wanawake mashujaa
uliofanyika leo kwenye ukumbi wa hoteli ya Haytt leo jijini Dar es
Salaam.
Alikuwa
mke wa marehemu Rais wa Msumbiji, Graça Machel akizungumza na wanawake
kuhusu namna ya mwanamke kujiamini pamoja na kufanya kazi ka bidii ili
kufikia malengo aliyojiwekea kwenye mkutano ulioandaliwa na Mtandao wa
Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana na taasisi ya GRACE MACHEL
FOUNDATION ya nchini Afrika Kusini.
Zaidi
ya washiriki 60 kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika wamekutana leo
jijini Dar es Salaam katika tukio la ana kwa ana na wanawake mashujaa
likiwa na lengo la kujadili na kuangalia changamoto zinazowakabili
wanawake.
Tukio
hilo limeandaliwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirikiana
na taasisi ya GRACE MACHEL FOUNDATION ya nchini Afrika kusini ambayo
inajishughulisha na shughuli zake barani Afrika ambalo litafanyika kwa
siku nne.
Akizungumza
katika tukio hilo mgeni rasmi Graça Machel amesema kuna haja ya
kuangalia ni nini kinafanywa na wanawake na kuangalia uchumi wa mwanamke
na umoja wa wanawake katika kutetea haki zao.
Naye Mama
Gertrude Mongella akizungumza katika tukio hilo amesema ili kuendana
na kasi ya maendeleo kwa mwanamke hakuna haja ya mwanamke kulalamika,
kuomba, kulia lia pamoja na kulaumu ili kuweza kuwapata wanawake wachapa
kazi.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP),
Bi. Lilian Liundi amesema wameamua kukutana pamoja ili kujitathmini
huku wakiangalia agenda mbili ya wanawake na ukatili wa kijinsia pamoja
na kuangalia haki ya uchumi na ushiriki wa wanawake katika uchumi.
Kupitia
tukio hilo viongozi hao mashuhuri watapata nafasi ya kuulizwa maswali
mbalimbali kutoka kwa washiriki wa tukio hilo ili washirikiki hao vijana
na wao kuona kuwa inawezekana kufikia hatua walizofikia viongozi hao.
Akizungumza
katika kongamano hilo kijana mwanaharakati kutoka Tanzania, Halima Lila
amesema "Hatuna mwongozo sahihi wakulinda elimu ya mtoto wa kike,bado
Kuna hitaji kubwa la kutoa elimu juu ya uzazi kwa vijana wakike na wa
kiume" amesema.
Seif
Ibrahim amesema Tanzania bado kuna tatizo la ajira kwa vijana na mimba
kwa watoto wakike ambao wengi wanashindwa kumaliza elimu zao za
sekondari lakini pia elimu zinazotolewa kwa vijana mashuleni haziwapi
uwezo wa kujitegemea wamalizapo masomo "amesema.
0 comments:
Post a Comment