Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Meneja
Mahusiano Kitengo cha Mikopo NMB, Emmanuel Mahodanga (kushoto) akiteta
jambo na Mkurugenzi wa Michezo na Utimamu wa Mwili wa Jeshi la Wananchi
Tanzania (JWTZ) - Kanali Richard Mwandike (kulia) katika hafla hiyo.Kaimu
Afisa Mkuu wa Wateja wadogo na Wakati wa NMB - Boma Raballa (kushoto)
akimkabidhi vifaa mbalimbali vya michezo Mkurugenzi wa Michezo na
Utimamu wa Mwili wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) - Kanali Richard
Mwandike (kulia) leo jijini Dar es Salaam. Vifaa hivyo mbalimbali vya
michezo zikiwemo jezi, mipira na vifaa vingine vyenye thamani ya
shilingi milioni 10, vitatumiwa na wachezaji wa timu ya JWTZ
wanaotarajia kusjiriki Mashindano ya Kijeshi ya Jumuiya ya Afrika
Mashariki yanayotarajia kuanza Agosti 24, 2017.
Kaimu
Afisa Mkuu wa Wateja wadogo na Wakati wa NMB - Boma Raballa (kushoto)
akimkabidhi vifaa mbalimbali vya michezo Mkurugenzi wa Michezo na
Utimamu wa Mwili wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) - Kanali Richard
Mwandike (kulia) leo jijini Dar es Salaam.
Vifaa
hivyo mbalimbali vya michezo zikiwemo jezi, mipira na vifaa vingine
vyenye thamani ya shilingi milioni 10, vitatumiwa na wachezaji wa timu
ya JWTZ wanaotarajia kusjiriki Mashindano ya Kijeshi ya Jumuiya ya
Afrika Mashariki yanayotarajia kuanza Agosti 24, 2017.Kaimu
Afisa Mkuu wa Wateja wadogo na Wakati wa NMB - Boma Raballa (kushoto)
akimkabidhi vifaa mbalimbali vya michezo Mkurugenzi wa Michezo na
Utimamu wa Mwili wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) - Kanali Richard
Mwandike (kulia) leo jijini Dar es Salaam. Vifaa hivyo mbalimbali vya
michezo zikiwemo jezi, mipira na vifaa vingine vyenye thamani ya
shilingi milioni 10, vitatumiwa na wachezaji wa timu ya JWTZ
wanaotarajia kusjiriki Mashindano ya Kijeshi ya Jumuiya ya Afrika
Mashariki yanayotarajia kuanza Agosti 24, 2017.Mkurugenzi
wa Michezo na Utimamu wa Mwili wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) -
Kanali Richard Mwandike (kulia) akimshukuru Kaimu Afisa Mkuu wa Wateja
wadogo na Wakati wa NMB - Boma Raballa (kushoto) mara baada ya kupokea
vifaa mbalimbali vya michezo leo jijini Dar es Salaam vilivyotolewa na
NMB kuwezesha timu ya JWTZ kushiriki Mashindano ya Kijeshi ya Jumuiya ya
Afrika Mashariki yanayotarajia kuanza Agosti 24, 2017.Kaimu
Afisa Mkuu wa Wateja wadogo na Wakati wa NMB - Boma Raballa (kushoto)
akimkabidhi vifaa mbalimbali vya michezo Mkurugenzi wa Michezo na
Utimamu wa Mwili wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) - Kanali Richard
Mwandike (kulia) leo jijini Dar es Salaam. Vifaa hivyo mbalimbali vya
michezo zikiwemo jezi, mipira na vifaa vingine vyenye thamani ya
shilingi milioni 10, vitatumiwa na wachezaji wa timu ya JWTZ
wanaotarajia kusjiriki Mashindano ya Kijeshi ya Jumuiya ya Afrika
Mashariki yanayotarajia kuanza Agosti 24, 2017.
BENKI ya NMB leo imekabidhi vifaa vya michezo kwa timu ya Jeshi la
Wananchi Tanzania (JWTZ) inayotarajia kushiriki Mashindano ya Kijeshi
ya Jumuiya ya Afrika Mashariki itakayofanyika jijini Bujumbura -
Burundi. Vifaa vilivyokabidhiwa leo ni pamoja na mipira kwaajili ya timu
ya mpira wa miguu, mipira ya mchezo wa mikono (wasichana) na mipira
mchezo wa kikapu kwa wanaume (Basket ball).
Akikabidhi
vifaa hivyo kwa Mkurugenzi wa Michezo na Utimamu wa Mwili wa JWTZ -
Kanali Richard Mwandike, Kaimu Afisa Mkuu wa Wateja wadogo na Wakati wa
NMB - Boma Raballa alisema vifaa vingine ni pamoja na mipira 10 ya
mchezo wa volebo (Volleyball), jezi 42 za mpira wa miguu, seti mbili za
jezi mpira wa kikapu (wasichana), seti mbili za jezi mpira wa basket na
seti mbili za jezi mpira wa Volleyball.
Vifaa
vingine vilivyokabidhiwa ni pamoja na seti mbili za jezi za waamuzi kwa
michezo ya Netball, Basketball, Volleyball na mabegi 30 ya wachezaji
ambapo vyote kwa ujumla vina thamani ya shilingi milioni 10 za
Kitanzania. Bw. Raballa alisema kuwa msaada huo umetokana na ushirikiano
mzuri na wa muda mrefu kati ya benki ya NMB na jeshi la wananchi
Tanzania (JWTZ) na ndiyo maana wakaona umuhimu wa kuendelea kuwashika
Mkono kupitia msaada kwa timu za jeshi zinazoenda kushiriki mashindano
ya majeshi ya jumuia ya afrika ya mashariki.
"...Hii
si mara ya kwanza kusaidia katika mashindano haya, kwani nakumbuka hata
mwaka jana tuliwasaidia baadhi ya vifaa vya michezo kushiriki katika
mashindano haya. Tunaamini vifaa hivi mbali na kuendeleza ushirikiano
wetu mzuri, vitakuwa chachu ya kufanya vizuri katika mashindano haya
muhimu kwa jumuia ya Afrika ya Mashariki," alisema Raballa.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi wa Michezo na Utimamu wa Mwili wa JWTZ - Kanali
Richard Mwandike akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya JWTZ alisema
anaishukuru NMB kwa msaada wa vifaa hivyo na kuongeza kuwa msaada huo
umewapa morali ya kufanya vizuri zaidi kwenye mashindano hayo. Kanali
Mwandike aliongeza kuwa timu hiyo itatumia jezi na vifaa vingine walivyo
kabidhiwa kwenye mashindano hayo huku wakiahidi kuwa mabalozi wazuri wa
NMB nan chi kwa ujumla. Kwa Mwaka wa 6 mfululizo, NMB imekuwa ikisaidia
timu za Majeshi wanapoenda kuwakilisha nchi kupitia michezo mbalimbali
na katika mashindano mbalimbali.
0 comments:
Post a Comment