Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mgombea urais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania (TFF), Shija Richard akizungumza na waandishi wa habari kuhusu namna atakavyofanya kampeni zake alizozizundua leo rasmi na akiahidi maendeleo ikiwemo na kujenga shule za akadeni ya kabumbu katika kanda sita 6 nchini.
Na Agness Francis, Globu ya Jamii.
Mgombea
wa Urais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania (TFF) Shija
Richard ameanza rasmi harakati za kufungua kampeni yake ya kuwania
nafasi ya urais wa shirikisho hilo hapa nchini.
Shija
amezungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam nia na
madhumuni ni kufungua rasmi zoezi la kampeni yake ambayo imejikita
kuzungumzia sera zaidi ya TFF badala ya maswala ya kiutendaji
Mgombea
huyo amesema kuwa atahakikisha kunakuwepo na sport Academi katika
kanda sita hapa nchini, hii itaongeza vipaji vingi vya kabumbu na
kuwashawishi wazazi wanapeleka watoto wao wenye vipaji katika shule
hizo za mafunzo ya mpira.
Hata
hivyo Shija amesema kumekuwa na tatizo kubwa kwa klabu kukosa kuwa na
uwanja, na hilo pia husababisha kutofanya vizuri kimataifa hivyo amesema
atahakikisha anatafuta wadhamini kujikita katika swala zima la miundo
mbinu ili kila klabu kujengewa kiwanja chake
Amesema
ili kucheza mpira kwa amani na utulivu bila kupendelea upande mmoja wa
timu ataweka mkakati kwa kushirikiana na vyama vingine vya michezo
duniani kote ili kuleta ufanisi kwenye mchezo huo hapa nchini.
Uchanguzi
huo unatarajiwa kufanyika tarehe 12 Agosti mwaka huu mjini Dodoma
ambapo wagombea hao wa kiti cha urais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu
nchini Tanzania (TFF) ni Shija Richard, Wallace Karia, Iman Madega, Ally
Mayay, na Emmanuel Kimbe.
0 comments:
Post a Comment