Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akiwa kwenye picha ya pamoja na Balozi wa Mauritius nchini Tanzania
Mhe. Jean Pierre Jhumun mwenye makazi yake mjini Maputo,Msumbiji ,
Wawekezaji wa Uzalishaji Sukari na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Profesa
Godius Kahyarara na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,
Bw.William Erio .(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akiagana na Balozi wa Mauritius nchini Tanzania Mhe. Jean Pierre
Jhumun mwenye makazi yake mjini Maputo,Msumbiji mara baada ya kumaliza
mazungumzo ofisini kwake Ikulu jijini Dar Es Salaam.(Picha na Ofisi ya
Makamu wa Rais)
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akiagana na Balozi wa Mauritius nchini Tanzania Mhe. Jean Pierre
Jhumun mwenye makazi yake mjini Maputo,Msumbiji aliyeongozana na
Wawekezaji wa Uzalishaji Sukari ambao wameonyesha utayari wa kuwekeza
nchini Tanzania.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo
amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Mauritius nchini Tanzania
Mhe. Jean Pierre Jhumun mwenye makazi yake mjini Maputo,Msumbiji
aliyeongozana na Wawekezaji wa Uzalishaji Sukari ambao wameonyesha nia
na utayari wa kuwekeza nchini.
Mbali
ya ujumbe kutoka Mauritius, wengine waliohudhuria mazungumzo hayo ni
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Profesa Godius Kahyarara na Mkurugenzi Mkuu wa
Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bw.William Erio .
Katika
mazungumzo hayo Makamu wa Rais amewahakikishia wawekezaji hao
ushirikiano wa Serikali na kuwaeleza kuwa Tanzania ina mazingira bora ya
uwekezaji.
Mbali ya fursa ya uwekezaji katika Sukari, Makamu wa Rais aliainisha maeneo mengine ya kuwekeza kama vile viwanda na TEHAMA.
Aidha
alisema pindi uwekezaji huo ukifanikiwa , Tanzania itafaidika na soko
la nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo ya
Kusini mwa Afrika (SADC) na masoko mengine duniani kwa ujumla.
Uwekezaji huu utakuwa wa Ubia kati mashirika ya hifadhi ya mifuko ya jamii na pia kampuni nyingine za wazawa.
0 comments:
Post a Comment