Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mkurugenzi
Mkuu wa Pizza Hut Afrika, Ewan Devenpot(Katikati) kwa pamoja
wakishangilia mara baada ya kukata utepe
kufungua Mgahawa wa Pizza Hut Mlimani City jijini Dar es Salaam leo.
Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Pizza Hut, Vikram Desai pamoja na
Meneja masoko wa Pizza Hut Tanzania,Bahati Komba.
Sehemu husika kwa wahusika watakaotembelea Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Amesema
kuwa ajira zilizopo ni katika viwanda vya mabox ambayo nao hutumia
katika kuandaa Pizza pamoja na viwanda vya chill source, Tomato source
ambapo kuna watu ambao wameajiliwa katika viwanda hivyo.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Pizza Hut, Vikram Desai na baadhi ya wateja wakionja pizza
zilizoandaliwa ikiwa kunapizza za nyama, mbogamboga pamoja na uyoga.
Pizza Hut
inamilikiwa na kampuni ya Dough Works Ltd, sasa kuajiri wafanyakazi zaidi ya 100 ambao ni
watanzania hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Pizza Hut, Vikram Desai wakati wa uzinduzi wa migahawa miwili iliyopo Mlimani City na Oysterbay jijini Dar es Salaam leo.
akizungumza katika uzinduzi wa migahawa hiyo amesema kuwa Mwaka huu mgahawa wa Pizza Hut ulitambulisha usambazaji bure wa
chakula katika ofisi na majumbani na hivyo kuwarahisishia huduma wateja wake.
Migahawa miwili ya Pizza hut ipo katika eneo la maduka la Mkuki, jengo la Peugeot na Shoppers
Plaza Mikocheni inaendelea kuhudumia mamia ya wananchi kwa chakula cha mchana
na usiku.
Migahawa ya
Pizza Hut ni ya kisasa ikiwa na sehemu ya watoto ya michezo mbalimbali, na
sehemu za kukaa za ndani na nje. Pamoja na kuwa na chakula kitamu aina ya Pizza
pia wametambulisha aina mbali mbali za bidhaa za kuku zenye ladha tofauti.
Zaidi ya mpango huo wa kupanua biashara kwa migahawa miwili zaidi kabla ya
mwisho wa mwaka pia tunaangalia uwezekano wa kufungua biashara katika mikoa ya
Dodoma, Arusha na Mwanza.
0 comments:
Post a Comment